Katika picha Profesa mbobevu wa Ikolojia kutoka SUA Prof. Pantaleo Munishi akiteta jambo na kutoa maelekezo kwa wanafunzi wakati wa mafunzo kwa vitendo Hifadhi ya Taifa ya Mikumi Mkoani Morogoro
Professor Robinson Mdegela of
@SokoineU
, Morogoro Tanzania, cordially invites you to attend his Professorial Lecture using the link below.
Topic: CATALYSING SOLUTIONS FOR ANTIMICROBIAL RESISTANCE IN TANZANIA USING ON HEALTH APPROACH
Time: Oct 26, 2022 02:00 PM Nairobi
SUA imefanya Mahafali ya 42 ambapo Wahitimu 3095 wametunukiwa vyeti vya kuhitimu Elimu ya Chuo Kikuu na Mhe. Jaji Joseph Warioba huku wakihudhurishwa kwa mara ya kwanza Wahitimu wa kwanza wa ngazi ya Shahada kutoka Kampasi ya Mizengo Pinda Mkoani Katavi.
@WizaraKilimo
@TCU
Mratibu wa Utafiti na Machapisho kutoka SUA Prof. Japhet Kashaigili ( Aliyevaa kofia) akiwa kwenye moja ya vitalu miche rafiki na maji vilivyoanzishwa na Mradi wake wa EFLOWS Mkoani Njombe kwa lengo la kurudisha uoto wa asili kwenye mito na vyanzo vya maji vya mto Mbarali.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Salvador Valdés wakishuhudia utiaji Saini wa Hati za Makubaliano kati ya SUA na Chuo Kikuu cha Artemisa cha Cuba, 24 Januari 2024, Ikulu Dar es salaam.
shangwe, nderemo na vifijo kwa Wanafunzi wa Shahada ya Sayansi ya Kaya na Taaluma ya Mlaji ( and Consumer Studies) wa mwaka wa tatu katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo baada ya kumaliza mitihani ya mwisho ya kuhitimu masomo yao.
NORWAY NA SUA KUDUMISHA USHIRIKIANO
Serikali ya Norway imeahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania kupitia Chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo ( SUA ) katika miradi mbalimbali ikiwemo kupambana na mabadiliko ya tabianchi.
Read More:👇👇👇👇👇👇
SUA imepokea Tuzo kwa kushika nafasi ya kwanza katika uandaaji na uwasilishaji wa taarifa bora ya mahesabu kwa viwango vya kimataifa kwa hesabu za 2021/22 kwa upande wa Taasisi za Elimu ya Juu nchini zilizoshindanishwa na Bodi ya Taifa ya Uhasibu na Ukaguzi Nchini (NBAA).
Mafunzo ya kuchakata mazao ya misitu yaiva SUA
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo kupitia Kituo chake cha mafunzo cha Olmontonyi Arusha, kimenunua mashine ya kisasa ya kuchakata magogo aina ya "Slidetec mobile sawmll" kutoka Finland.
Ndaki ya Kilimo, Idara ya Lishe na Sayansi ya Mlaji imekutana na wadau wakiwemo waajiri kutoka Sekta za Umma na Binafsi katika kikao cha kuboresha mitaala programu zinazofundishwa na Ndaki hiyo, lengo ni kuona mitaala mipya inagusa mahitaji muhimu ya sasa katika kumuandaa mhitimu
Sokoine University of Agriculture (SUA) has signed a cooperation agreement with Mwalimu Julius Nyerere University of Agriculture and Technology (MJNUAT) for academic collaboration and faculty exchange. The agreement was signed in Morogoro.
#Education
#Collaboration
Baadhi ya vijana waliopata ajira ya muda kupitia Mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) wakiwa katika picha ya pamoja na Rasi wa Ndaki ya Kilimo Dkt. Nyambilila Amuri baada ya usaili uliofanyika Ukumbi wa Multipurpose Kampasi ya Edward Moringe, Morogoro.
Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga SUA wameaswa kufuata utaratibu pindi wanapokumbana na changamoto.
Hayo yamebainishwa na Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Raphael Chibunda wakati akiwakaribisha na kuwapongeza kwa kuchaguliwa SUA.
Timu ya Mpira wa Miguu ya Wanafunzi ya SUA imepokelewa kwa kishindo na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo upande wa Mipango, Fedha na Utawala, Prof. Amandus Muhairwa mara baada ya kuwasili na taji katika soka kwa kukifunga Chuo Kikuu cha Ardhi bao 2-1 katika Mashindano ya TUSA.
Karibu umsikilize Prof. Amandus Muhairwa, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo upande wa Mipango, Fedha na Utawala akielezea SUA ilivyo Benki ya Wataalamu na taswira halisi ya Chuo hicho baada ya miaka michache ijayo.
@ViwandaBiashara
@WizaraKilimo
@wizarayaelimu
@WizaraYaAfya
Baadhi ya Wanafunzi wanaoendelea kuripoti SUA kwa ajili ya kuanza masomo ya mwaka wa kwanza 2023/2024 wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri Mkuu wa Serikali ya Wanafunzi hapa Chuoni Ndg. Lusotola Philipo baada ya kupokelewa katika Stand ya Msamvu, Morogoro tarehe 23.10.2023.
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimeibuka kidedea kwa kuwa mshindi wa kwanza kwa kundi la vyuo vikuu na vyuo vya kati na mshindi wa pili wa jumla katika maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki.
Baadhi ya wanafunzi wasichana wa SUA wamesema kutokana na kuaminiwa kwa wanawake katika uongozi kumeongeza ushiriki wa wanawake katika masuala ya maendeleo kiuchumi.
Wanafunzi wa kidato cha kwanza watarajiwa wa Shule ya Sekondari Forest Hill Morogoro wakifuatilia maelekezo yanayotolewa na Stella Genge Afisa Mafunzo Kitengo cha Ukuzaji Viumbe Maji kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo walipofanya ziara ya kujifunza chuoni Novemba 30, 2023.
Wananchi na Viongozi mbalimbali wameendelea kutembelea katika banda la SUA kwenye maonesho ya wiki ya Ubunifu yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.
Maonesho hayo yanafanyika katika Uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma yaliyoanza tarehe 24 Aprili, 2023.
Makamu Mkuu wa Chuo cha SUA Prof. Raphael Chibunda (wanne kutoka kulia kwa waliosimama mstari wa kwanza), katika picha na Rais wa JMT Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Makamu Wakuu wa Vyuo vya Umma baada ya kumalizika kwa kikao Ikulu tarehe 29 Septemba, 2023
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof. Raphael Chibunda akibadilishana zawadi na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Artemisa cha Cuba Dkt. Adianez Bermundes alipofanya ziara ya siku moja SUA ukiwa ni mwanzo wa ushirikiano wa Vyuo hivyo, leo tarehe 25.01.2023.
SUA kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo katika Utekelezaji wa Programu ya BBT wanawaarifu Waombaji wa nafasi za ajira za muda kupitia program maalum ya kuendeleza zao la pamba nchini kuwa wanaitwa kwenye usaili.Kwa taarifa zaidi fungua link hapo chini.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amefanya ziara katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Novemba Mosi, 2023 ili kujionea eneo la Kituo Atamizi pamoja na Jengo Mtambuka la Mafunzo.
Baadhi ya wafugaji kutoka mikoa mbalimbali wanaoshiriki mafunzo ya ufugaji bora wa kuku yanayoratibiwa na Taasisi ya Elimu ya Kujiendeleza ya SUA wakiendelea na mafunzo kwa vitendo kwa kuwatembelea wafugaji kuku mkoani Morogoro na kujifunza namna wanavyofuga, Januari 31, 2024.
SUA and NMBU signed an MoU to renew collaboration, an event witnessed by H.E. Samia Suluhu Hassan, President of the United Republic of Tanzania and the Norwegian Minister of International Development Hon. Anne B. Tvinnereim.
@ikulumawasliano
@WizaraKilimo
@UniNMBU
Applications are hereby invited for admission into Higher Degrees at Sokoine University of Agriculture (SUA) for the academic year 2020/2021. Click the link below for more informatin