SUA imepokea Tuzo kwa kushika nafasi ya kwanza katika uandaaji na uwasilishaji wa taarifa bora ya mahesabu kwa viwango vya kimataifa kwa hesabu za 2021/22 kwa upande wa Taasisi za Elimu ya Juu nchini zilizoshindanishwa na Bodi ya Taifa ya Uhasibu na Ukaguzi Nchini (NBAA).