Nikiwa Mtwara kutengeneza kipindi cha TV na wasichana kuhusu mimba za utotoni,niliwahoji baadhi ya wasichana kuhusu kujitunza wakaniambia “Sisi tumepewa bure kwanini tuwanyime?”
Hili jibu linaweza kukupa picha ya ujumla kuhusu tatizo la kujitambua,malezi na tamaduni kwenye jamii
Huyu DC achukuliwe hatua kali, pamoja na kuwa ukatili haukubaliki kipindi chochote, lakini ana uthubutu wa namna gani kumpiga binti hadharani kabisa kwenye siku 16 za kupinga ukatili???.
Pia ni kukosa maadili ya uongozi
@maendeleoyajami
@Dr_DGwajima
@MwananchiNews
@TheChanzo
Kaka yangu
@AllyHapi
lugha kama hizi za kuobjectify wanawake tena zikitoka kwa viongozi wetu zinaturudisha sana nyuma. Tunasema ni mzaha lakini hakuna mzaha kwenye lugha za kudhalilisha wanawake.Tuheshimu taaluma za wanawake na kuweka weledi mbele
“...we find and hold that the entire appeal has no merit.The appellant was supposed to abide by the order of the High Court to cause the amendment of the LMA as directed.Having so stated,we dismiss the appeal in its entirety with no order as to costs” Pg 51 of CAT’s ruling
Ninamshukuru Mungu kwa neema ya uzima,leo nimeongeza mwaka mwingine kwenye maisha yangu. Nawashukuru watu wote mliowahi kuwa sehemu ya maisha yangu katika nyakati tofauti tofauti,hakika mna mchango mkubwa katika kunifanya niwe jinsi nilivyo leo 🌺
Hii picha kwangu ina maana kubwa, huyo mama mstari wa pili upande wa kulia ni zaidi ya malaika kwangu,wakati nimefaulu kwenda Kilakala 2006 aliniita ofisini kwake akanifanyia shopping ya kila kitu cha shule😭,wazazi hawakuwa na Angel is getting a PhD 🙌🏾🙌🏾
Hon. Deputy Minister of Agriculture, Dr. Mary Mwanjelwa & other PhD graduates listening to various speeches during the 37th graduation ceremony of the Open University of Tanzania held on 28th September 2019 at Bungo, Kibaha.
My sincere appreciation to this panel of advocates who represented our case at the Court of Appeal
1)
@Advocate_Jebra
2) Senior Adv. Mpale Mpoki
3) Adv.
@fulgencem
4)Adv. Alex Mgongolwa
5) Adv. Mary Richard
#ndoazautotoni
Muasisi wa Shirika la Msichana Initiative, Rebeca Gyumi ametajwa kama mmoja ya Wanawake 100 wenye ushawishi duniani. Orodha hii huandaliwa kila mwaka na
@BBC
kwa kuangalia wanawake ambao ndani ya miezi 12 wamekuwa sehemu ya mazungumzo ambayo yameleta mabadiliko katika jamii zao.
Nawashukuru sana watanzania wenzangu kwa salamu za pongezi. Habari hii kwangu na wenzangu kupitia shirika ninaloliongoza imetupa hamasa zaidi ya kuongeza nguvu kwenye kufanyia kazi masuala ya wasichana.Namshukuru Mungu,hakika si kwa uwezo wangu bali ni kwa yeye anitiaye nguvu.
Kama kuna kitu tunatakiwa kupaza sauti kwa pamoja bila kujali itikadi, makundi n.k ni ulinzi wa Katiba yetu na utawala wa sheria. Tukatae double standards
Sisi wenyewe ndio tumesema wasichana wenye mimba wasirudi shule, mkopo tumeomba wenyewe, now habari inasambaa kuwa hatutapewa huo mkopo tena, tunaanza laumu kuwa kuna watu wanatumika. How?? Tunafikiri tunaishi kwenye kisiwa kwamba tukifanya jambo halionekani??
Ndugu zangu,watanzania wenzangu na wote ambao mmechukua muda wenu kunipongeza nasema AHSANTE 🙏🏾.Tuendeleze jitihada za kuhamasisha haki katika jamii zetu.Nitumie pia fursa hii kutambua wapigania haki za binadamu wengine ambao hatuwasikii,mnachofanya kina umuhimu sana,msichoke ✊🏾
Moja ya kauli naipenda kutoka kwa Bibi Titi ni pale alimuuliza Mwl. Nyerere,Mbona wanawake hawaonekani kwenye nafasi za maamuzi Mwl?.Mwl akamuuliza “Wanawake wenye uwezo wako wapi Bibi Titi?”,Bibi Titi akajibu “Kwani wanaume wenye uwezo mmewapataje?”
NB: Wanawake wenye uwezo wapo
Mh. Rais mwenyewe alishawahi muita kijana mchekeshaji aigize sauti yake tena akiwa amepanda juu ya gari analotembelea akiwa Mafinga kama sikosei. Tusikose uvumilivu kiasi hicho hata tushindwe kutaniana na kucheka jamani?
Leo nilipata mwaliko wa kuonana na Mh. Rais Samia Suluhu Hassan, kuongea na kushauriana kuhusu masuala kadha wa kadha. Mchango wangu pamoja na mambo mengine ulijikita kushauri kwenye maeneo ya upatikanaji wa elimu hasa kwa mtoto wa kike 1/2
Kuanzisha jambo,kulisimamia na likafanikiwa sio jambo rahisi.I've personally had so many bad days than good, but kila siku unajipa moyo kesho ni njema kuliko jana. Na ni ngumu zaidi kama hauna solid support system inayokupa nguvu unapotaka kukata tamaa, cause stress ni nyingi 😞
Kwanini viongozi hawataki kutekeleza jukumu lao la kuongoza? kuweka na kusimamia mipango ya kunusuru uchumi na ya kupunguza maambukizi? wote tunaimani lakini tulichagua viongozi kwa sababu, lead us.
Tunawezaje hamasisha watu kuchangia maendeleo wakati kila mwaka wanaona ripoti za ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha ya umma?? nchi yetu haina tatizo la mapato,tuna shida kubwa ya matumizi,kuendelea kuminya wananchi wa kawaida kupitia tozo hakutaleta suluhu,kamwe!
Ujumbe waliotuma wanawake wa marekani kwa Rais wao umesikika, wameweka historia ya kugombea wanawake wengi kuliko wakati wowote na kushinda viti walivyogombea. Walisema kama Rais wetu hapendi wanawake basi tutagombea kumuonesha uwezo wetu
Kuna tofauti ya mtu aliyesoma na mtu aliyeelimika, bahati mbaya sana nawiwa kusema kwa jinsi ambavyo nimekuwa naona tweets za Niki wa pili wiki hii anaweza kuangukia kwenye kundi la kwanza 🤦♀️
Ushauri Waajiriwa (hasa vijana):Kuwa mwangalifu sana na mtu anayekwambia vitu vibaya au kukukatisha tamaa kuhusu ofisi uliyopo ila yeye yuko hapo miaka yote,anaweza hata kukupa michongo ya kuomba kazi sehemu nyingine,ila yeye haachi kazi,my dear, za kuambiwa changanya na zako😂
Tumesikitishwa sana na kitendo cha ubakaji alichofanyiwa binti wa miaka (14) na vijana wanne eneo la Pugu Migombani, Ilala na kupelekea kupoteza maisha. Wasichana wangapi watakufa ili tuseme
#INATOSHA
??
#IAMHER
Prof. akiwa mwalimu wangu wa Sheria Mlimani alikuwa mmoja ya watu waliotupa hamasa sana kufanyia kazi hii sheria ili kulinda wasichana wakati wa somo la Family Law. Nafikiri busara ni kutoongea wakati wa kula kama huwezi simamia misingi uliyoiasisi
Video za kinachoendelea kwa wenzetu wa Zanzibar zinajenga taswira mbaya kwa taifa letu. I condemn the acts in strongest term possible
#ZanzibarLivesMatter
Hili neno mabaharia na sifa zake linanikumbusha wakati tupo sekondari, shule ya Kikuyu, Dodoma kulikuwa kuna kundi linajiita “wakongwe”, walikuwa na sheria za ajabu 😀, mara wakongwe hawaogi, wakichapwa hawatoi machozi, mkongwe hachomekei 😅😅
@___gillian____
👉🏾Tunakataza ngono na watoto chini ya umri wa miaka 18
👉🏾Tunafunga watu wanaowapa mimba wanafunzi
👉🏾Lakini tunaruhusu wasichana chini ya umri wa miaka 18 kuolewa.
👉🏾 Sasa badala ya kuozea jela kwa kumpa Msichana mimba,NAMUOA,nakuwa nimeepuka adhabu na bado naendelea na ngono
Ni neema kuongeza mwaka mwingine kwenye maisha. Ni dua yangu kila ninapoendelea kubarikiwa na neema ya uzima, Mungu azidi kukamilisha kusudi lake kupitia maisha yangu 🙏🏾, yote kwa utukufu wake.
Katika maisha hata siku moja usiruhusu uwezo wako kifedha,elimu, maarifa kukufanya ujione bora kuliko wengine.Ishi kwa kushirikiana na wengine na siku zote chanzo cha kushirikiana ni UPENDO.Maana ukiwapenda watu huwezi kujiona bora zaidi/kuliko.
Miaka michache nyuma tulipata bahati kama viongozi vijana kualikwa kwenye mazungumzo na Mh. Benjamin William Mkapa,tulizungumza kwa kina kuhusu masuala ya VVU/UKIMWI na elimu kwa mtoto wa kike. Mh. Mkapa alikuwa ni championi wa AIDS FREE GENERATION, pumzika kwa amani 🙏🏾
“...Mtoto wa miaka 18 bado ni mtegemezi kwa mzazi wake...” nakubaliana na wewe kabisa Mh. Rais
@SuluhuSamia
, lakini mtoto huyu huyu akiwa na miaka 14, Sheria yetu inamtwika majukumu mazito ya ndoa na kuhudumia familia. Tunahitaji mabadiliko kwenye hili pia Mh .Rais
Comments za baadhi ya wanaume kwenye post hii ya Hellen,SMH 😏.Hellen ni ushuhuda wa nguvu ya 2nd chance kwa wasichana wanaoshindwa kuendelea na masomo sababu ya ujauzito.Lugha mlizotumia mngekuwa mnatumia hizo hizo kwenye kukemea wanaume na wavulana wanaofanya ngono na wanafunzi
Pia nisisitize, sio lazima kila mtu unayemuona anatetea jambo fulani au hatetei basi amelipwa au anatumika. Hayo ni mawazo mufilisi, tujenge nchi yetu kwa kupeana uhuru wa kujadiliana kwa hoja
Idadi ya hapana na “rekebisha kwanza ndio utume tena” nilizopata mwaka huu, hazinikatishi tamaa. Nazitumia kunipa nguvu na kujenga ngazi za kufika napotaka, one day Yes 🙏🏾
Msichana amevaa nguo fupi inaonesha asilimia kubwa ya maungo yake, inaweza kuwa ni RIDHAA ya kutoka kutongozwa au kufanya ngono??
#KizaziChenyeUsawa
#16DaysOfActivism
Nasikitishwa sana na matumizi ya lugha za matusi,na kwa sababu walengwa wamenielewa sitajibu. Kwenye tuhuma ukiacha mleta tuhuma anayetuhumiwa ni muhimu pia aseme upande wake and that’s all I asked from the institution.Hayo mengine ni yenu
Wakati mwingine ni kushukuru tu Mungu, kuna matukio yanakufanya ujue rangi halisi za watu,ili siku nyingine ujue sio wote wanaokutakia mema.Thats life 😊
Inahuzunisha kusoma kifo cha msichana nchini Kenya sababu ya “period shaming”.Kupata hedhi ni suala la kusherehekewa na sio kuonewa aibu au kudhihakiwa. Tuvunje hii “taboo” ya kuweka usiri/uchafu kwenye kupata hedhi. BILA HEDHI HAKUNA MAISHA
Habari za miili ya watoto iliyookotwa huko mkoani Njombe ikiwa imekatwa sehemu za miili yao ni za kusikitisha sana. Ni unyama tunaotakiwa kuukemea kwa nguvu zetu zote.
Tuko tayari kwenye Court room no 1 hapa Mahakama ya Rufaa tukisubiri kusomwa kwa uamuzi wa kesi ya
#NdoazaUtotoni
, fuatilia akaunti ya
@MsichanaUwezo
kwa update ya kinachojiri.
Wadau wanasubiri champagne 🍾 mtoto aliyezaliwa leo akapotea nayo mazima 😂😂😂. Ahsante mme wangu kwa zawadi na kila kitu yani, okhore bhuya mkurya wangu 😀😀
Tupunguze matumizi ya Serikali, tuoneshe kwa vitendo kushughulikia in a "zero tolerance" manner, wapigaji wote. Otherwise hata hizi tozo zitaenda kuwanufaisha wachache (tabaka tawala) at the expense of the majority poor people.
Wanangu njooni niwasimulie hadithi,
Hadithi ya maono ya mama yenu,
Hadithi ya kuamsha yaliyo ndani yenu,
Hadithi ya kuwakumbusha njia Zenu,
mliochoka mje,mpambane, muanze tena upya,
Wanangu kwakua mmekuja, nisikizeni,
Idadi ya watu walionifuata kwenye DM imenifanya nijiulize sana, RUSHWA YA NGONO ni tatizo kiasi hiki??? Tunafanyaje kuchallenge POWER? Maana mara nyingi rushwa ya ngono huhusisha watu wenye nguvu kutushinda be it shuleni, sehemu za kazi, biashara, siasa etc
I’m not a relationship expert,Ila nawiwa tu kusema na wewe,haijalishi unapitia kwenye changamoto gani za mahusiano wakati huu,Mungu wetu ni mwaminifu kwa wakati wake atakukutanisha na mtu wako atakayekupenda kama ulivyo.Amini katika muda wa Mungu, huwa hawai wala hakawii.
Hongera for such a milestone, napendekeza udonate kwa
@BintiSalhaFound
kupitia campaign yao ya
#HerEducation
ambapo wanachangia uniform kwa wanafunzi kutoka kwenye mazingira magumu.With your support they’ll reach many. Help me RT this TOT 🙏🏾
🥳 Thank you for 1 million followers on Twitter today! To mark this day, I will donate TZS 1 million (or more) to charitable causes / initiatives or businesses in need. Top 10 worthy causes with the highest retweets will be rewarded 🙏🏽
#MoGifts2020
Naomba nitumie ukurasa wangu leo kupongeza juhudi za mkuu wa mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri kwenye suala la Ndoa na mimba za utotoni, anaonesha high political commitment na kuchukia suala la watoto kuolewa na kupata mimba 1/2
Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana; Wote wenye mwili na walihimidi jina lake takatifu milele na milele. Zaburi 145:21
Muwe na Jumapili njema wapendwa katika bwana!
I am learning to always be conscious of my privileges and power. That I should not be in a space and claim to speak on behalf of an entire group or community of people while I might not necessarily be the average representation of the group,community etc 💡