4th President of Tanzania| Chancellor, University of Dar-es-Salaam| Chair, GPE Board| Co - Chair, HLC on
#ICPD25
| Chair, SADC Panel of Elders (PoE)| Chair, JMKF
Nimefarijika sana leo nikiwa Bagamoyo kukutana na Mwalimu Calistus Nazari aliyenifundisha darasa la 6 Lugoba Middle School mwaka 1963. Nimefurahi kumuona ana afya njema na nguvu pamoja na kuwa na umri wa zaidi ya miaka 80.
What a wonderful bird's eye view of our beautiful Mount Kilimanjaro, I was able to capture today February 12th, 2020. I was on a TGFA flight from Nairobi to Dar es Salaam. I have never been this lucky before and I have seen this much snow.
Nimetumia wikiendi yangu kumtembelea Mwalimu Raphael Semindu Simon aliyenifundisha darasa la kwanza katika shule ya Msingi Msoga mwaka 1958. Nimefika nilipofika kutokana na mchango wake adhimu.
Nimetoka kuwatembelea wakazi wangu wapya (tausi) katika makazi yangu hapa Msoga. Wamefika salama na 'wanajisikia nyumbani'. Namshukuru Mheshimiwa Rais
@MagufuliJP
kwa zawadi yake hii kwangu.
Nimepata tabu kuandika kwa kifupi kuelezea simanzi na masikitiko yangu kwa msiba mkubwa ulioukumba nchi yetu kwa kuondokewa na mpendwa wetu Mheshimiwa Rais
@MagufuliJP
. Nimelazimika kuyaambatisha hapa chini. Mwenyezi Mungu amuweke mahala pema, peponi.
Nimepata wasaa wa kutazama
#SlayOnNetflix
na kumuona
@IdrisSultan
katika sinema hii. Nimefarijika sana na hatua hii aliyopiga. Ametuweka Watanzania kwenye uso wa
#Netflix
. Ni mwanzo mzuri sana. Tumuunge mkono afanye vizuri zaidi, na azidi kututoa kimasomaso huko mbeleni.
Happy Birthday
@SuluhuSamia
. I wish you long, healthy and fulfilling life. On this auspicius day, please receive heartly congratulations on the wonderful work you're doing for our dear country, at home and abroad. Please continue the good work! We support you and we'll always do.
It is always my pleasure to catch up with my brother
@GEJonathan
. Unlike the past, today, there were less security details, less protocols, no formal agenda and no official photo. Life after Presidency sounds so cool. More freedom, more real!
Nimepokea kwa masikitiko na huzuni kubwa taarifa ya kifo cha mzee wetu Job Malecela Lusinde.Mmoja wa mashujaa wa kudai Uhuru wa nchi yetu na ujenzi wa taifa letu changa hatunae tena. Daima tutamkumbuka kwa mchango muhimu alioutoa kwa ajili ya nchi yetu.
Napenda kuwajulisha na kuwapa tahadhari kuwa akaunti ya
@KikweteMrisho
inayotumia picha na utambulisho unaotaka kufanana na wangu si akaunti yangu, wala si ya mtu ninayehusiana nae. Sihusiki na ujumbe wala maudhui yake. Chukueni tahadhari mnaposambaza ujumbe unaotokana nayo.
Kuna siku nilimsihi
@MwanaFA
na wanamuziki wengine kufanya shughuli nyingine zaidi ya muziki pekee. Nimefarijika leo kunitembelea na kutambulisha bidhaa yake mpya ya “body spray”. Hii ni hatua kubwa na nzuri kwa vijana wetu. Tuwaungishe!
Nimelemewa! Nakosa maneno ya kuelezea huzuni na majonzi niliyonayo kwa kifo cha Ruge Mutahaba. Taifa limepoteza kijana wake mahiri, mbunifu na mzalendo wa kweli. Nimepoteza rafiki, mshirika mwaminifu na mtu ambaye amenisaidia kwa mengi ktk uongozi wangu na hata baada ya kustaafu.
Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mzee Hassan Nasoro Moyo. Tumepoteza mmoja wa viongozi wetu mashuhuri. Atakumbukwa daima kwa mchango wake muhimu katika kuendeleza Mapinduzi ya Zanzibar na kudumisha Muungano wetu. Innalillahi Wainna Ilaihi Rajioun.
Nimestushwa na taarifa za kifo cha msanii wa kizazi kipya GodZila. Alikuwa kijana mdogo mwenye ndoto kubwa na ameondoka wakati ambapo bado mchango wake ulihitajika. Nawapa pole familia ya Marehemu na wasanii wote kwa msiba huu. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema.
Nimeitikia wito wa Serikali na Mhe Rais
@MagufuliJP
wa kusajili laini za simu kabla ya tarehe 20 Januari, 2020. Nimekamilisha kwa kusajili laini yangu ya mwisho leo. Namshukuru Obrien kutoka
@Tigo_TZ
kwa kunisajili. Nawahimiza na wengine kufanya hivyo kwai siku zimebaki chache.
Leo nimewatunuku Shahada za Kwanza wanafunzi wapatao 4,298 wa
@udsm
. Kati yao, wanawake ni 1,973 sawa na asilimia 45.9. Nilifarijika zaidi kuona katika wahitimu wawili, Bi. Edna Meela na Irene Msengi miongoni mwa walioongoza kwa GPA kubwa.
Kwa heri Mzee James Mapalala. Utakumbukwa daima kwa mchango wako muhimu uliotoa katika kukuza na kuendeleza demokrasia ya vyama nyingi nchini. Kapumzike kwa Amani. Ameen
Happy Birthday to Your Excellency President
@SuluhuSamia
. May you live a long, healthy, happy and fulfilling life. May God Almighty shower His bountiful blessings unto you as you steer the affairs of our great nation. May He answer your dreams for our country and its people.
I received the news of the passing on of former President Kenneth Kaunda (KK) with shock and a deep sense of sadness and sorrow. I convey my heartfelt condolence and sympathies to Your Excellency President
@EdgarCLungu
, KK's family and the friendly people of Zambia.
Leo nimejumuika na wananchi wenzangu wa Msoga kwenye Mkutano wa Kujadili Mpango wa Matumizi ya Ardhi (2019-2029) wa Kijiji cha Msoga. Kwa sisi wastaafu tunaoshughulika na shughuli za kulima na kufuga, kikao hiki kinahusu hatma yetu.
I congratulate you President
@UKenyatta
for being reelected as President of Kenya. I thank you for the invitation to attend your inauguration. I regret I will not be able to make it due to a prior commitment. I wish you all the best and success in your second term.
As a long-time champion of quality education for all, I am honored to be appointed as the new Board Chair of
@GPforEducation
. I look forward to helping GPE and partners transform education and address the global learning crisis.
Leo mimi na mke wangu Salma tulipata fursa ya kushiriki sherehe za mbio za Mwenge wa Uhuru. Nimeshiriki sherehe nyingi za Mwenge lakini hizi za kijijini zina hamasa yake tofauti.
Nimepokea kwa huzuni kubwa taarifa ya kifo cha ndugu yetu Dkt. Mengi.Taifa limepoteza mzalendo wa kweli na mfanyabiashara mahiri. Tutamkumbuka kwa mchango wake mkubwa aliyoutoa kwa maendeleo ya taifa letu na moyo wake wa upendo na huruma kusaidia jamii na hasa watu wasiojiweza.
Having lunch with kith and kin at the Uncle Said Lumaliza's (1917-2018) funeral at Msigi Village near hometown Msoga. This is a beauty of life after Presidency!
Nimewalisi Abuja, Nigeria kuongoza Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Madola kwenye Uchaguzi Mkuu wa Nigeria unaotarajiwa kufanyika tarehe 16 Februari 2019 kufuatia ombi la Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola.
Majonzi yangali nasi, nimepokea taarifa ya kifo cha Mtangazaji Ephrahim Kibonde wa
@cloudsfm
. Ni pigo kubwa kwetu sisi wapenzi wa kipindi cha Jahazi. Jahazi litaeleaje bila ya Nahodha Kibonde? Mwenyezi Mungu na aipe faraja familia yake,
@cloudsfm
na wasikilizaji wote wa Jahazi.
Mdogo wangu Mwanaisha Mrisho Kikwete ni miongoni mwa wanafunzi walitunukiwa shahada zao leo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Nimemtunuku Shahada ya Uzamili katika Elimu.
Algeria and Argentina are officially malaria-free! Congratulations on achieving
@WHO
certification and ensuring that your citizens are protected as we work to
#EndMalaria
globally.
Poleni sana Mwenyekiti Ibrahim Lipumba na wanachama wa CUF kwa msiba mkubwa wa Mheshimiwa Khalifa Khalifa uliowakuta. Ni msiba wetu sote. Mmepoteza kiongozi na Kada wa CUF wa kuaminiwa na kutumainiwa. Mimi nimepoteza rafiki wa muda mrefu.
Nawapongeza Zanzibar Heroes kwa kututoa kimasomaso na kutinga fainali. Nawatakia kila la kheri katika mechi ya fainali waibuke na kombe na watupe raha ambayo Watanzania tumeikosa kwa muda mrefu.
Naungana na wananchi wenzangu wote kukumbuka mchango adhimu wa Hayati Abeid Amani Karume, Muasisi wa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Muasisi wa Muungano, Rais wa kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Makamu wa Rais wa Tanzania. Tumuenzi daima kwa mchango wake uliotukuka.
Namshukuru Mzee wangu na Mlezi wangu Mheshimiwa Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi kwa kunitakia heri katika siku yangu ya kuzaliwa na kwa kuniimbia wimbo. Daima namshukuru kwa imani yake, malezi yake na upendo wake kwangu.
Nakupongeza Rais
@UKenyatta
kwa kuchaguliwa tena kuongoza nchi rafiki ya Kenya. Nakushukuru kwa mwaliko wa kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwako. Nasikitika sitaweza kuhudhuria kutokana na kuingiliana kwa majukumu. Nakutakia kila la kheri katika awamu yako ijayo.
Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Kapteni Dkt. Jaka Mwambi. Kapteni Mwambi nimetoka naye mbali. Nimesoma nae sekondari, Chuo Kikuu, Chuo cha Kijeshi Monduli na kada mwenzangu TANU na
@ccm_tanzania
. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema, peponi.
Kwa nyakati tofauti leo nimekutana na wagombea Urais wa Kenya
@RailaOdinga
, akiambatana na
@MarthaKarua
, na
@WilliamsRuto
. Tumekuwa na mazungumzo mazuri na wamenihakikishia wako tayari kusimamia misingi ya uchaguzi wa Haki&Uwazi kwa manufaa ya Taifa la Kenya na ustawi wa
@jumuiya
Nimesikitishwa na kuhuzunishwa sana na taarifa za kifo cha aliyekuwa mmoja wa wasaidizi wangu Dkt. Weggoro C. Nyamajeje. Naiombea familia yake moyo wa subira na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.Mwenyezi Mungu ampumzishe ndugu yetu mahala pema peponi.
Nilifarijika sana jana kukutana na maveterani na marafiki zangu wa zamani wa klabu yangu ya
@Yanga1935
katika maziko ya mchezaji wetu wa zamani, Marehemu Athuman Chama katika makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam.
On behalf of the End Malaria Council, I was pleased to meet with leaders of Africa's RECs in Addis Ababa. The Council will work closely with RECs to scale the war against malaria from Malaria control to Malaria elimination.
Kufuatia ombi la Kamishna wa Masuala ya Kisiasa wa Umoja wa Afrika (AU) nimewasili Afrika Kusini kuongoza ujumbe wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi wa AU kwenye Uchaguzi Mkuu wa Afrika Kusini unaotarajiwa kufanyika tarehe 8 Mei 2019.
I spared some time to watch
#SlayMovieOnNetflix
and I was delighted to see
@IdrisSultan
featuring in it. I congratulate him for being the first Tanzanian to feature on
#Netflix
and looking forward to seeing more of him in the future.
Tukila chakula na ndugu zangu msibani kwa baba yangu mdogo marehemu Said Lumaliza(1917-2018) katika kijiji cha Msigi karibu na Msoga. Hii ndiyo fahari ya maisha ya kustaafu.
Nimefarijika kusherehekea miaka 43 ya kuzaliwa kwa
@ccm_tanzania
kwa kutembelewa na maofisa wa Chama kuchukua maoni yangu juu ya mwelekeo wa Sera za Chama na Ilani ya Uchaguzi ujao.
Nimetembelea Maktaba yetu mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam baada ya mkutano wangu na Wajumbe wa Baraza la Chuo Kikuu. Nimefarijika sana. Ni ya viwango vya kimataifa. Nimetamani na kukumbukia enzi zangu nikiwa Mwana UDSM na Rais wa DUSO Kampasi ya Mlimani.
"Innalillah Wainna Ilaihi Rajiun. Kwa heri kaka yangu Mhe. Bakari Mwapachu. Daima tutakukumbuka kwa moyo wako wa upendo, huruma na ucheshi.Vile vile utakumbukwa kwa mema mengi uliyoifanyia nchi yetu na watu wake na kwa mchango muhimu uliotoa kwa ujenzi wa taifa letu.
Honoured to have witnessed the signing ceremony of the Peace and Reconciliation between the goverment of Mozambique and RENAMO in Maputo. I congratulate President Nyusi and leader of the RENAMO Ossufu Momade for their exemplary and selfless leadership.
Namshukuru
@OfficialAliKiba
kuja kunitembelea na kunitaarifu kuwa anatarajia kuoa hivi karibuni. Nimempatia nasaha zangu na kumtakia kila la kheri kwa jambo hilo jema aliloamua kufanya.
Mapema leo tukimpokea Makamu wa Rais Mheshimiwa
@SuluhuSamia
na Mjumbe wa Kamati Kuu ya
@ccm_tanzania
katika harambee ya chama mkoa wa Pwani. Tumeitikia wito wa viongozi wetu kuepuka kusalimiana kwa kushika mkono ili kuepuka maambukizi ya virusi vya
#coronavirus
. Tuitikie wito!
Natoa pongezi nyingi kwa IGP Simon Sirro na
@tanpol
kwa kuwakamata watu waliokuwa wanatumia vibaya jina langu, la mke wangu Salma na mwanetu Ridhiwani kuwahadaa na kuwaibia Watanzania ninaowapenda sana. Kubainika kwa mtandao huo na kukamatwa ni hatua nzuri ya kupongezwa.
Nimepokea kwa mshtuko na huzuni kubwa taarifa ya kifo cha Comrade Mohamed Seif Khatibu. Nimepoteza rafiki wa karibu wa tangu ujana hadi uzee wetu. Tumefahamiana nae tangu 1982 tulipochaguliwa kwenye uongozi wa taifa wa
@uvccm_tz
Nikiwa Boston nimekaribishwa na kupata wasaa wa kubadilishana mawazo na wanafunzi wa Tanzania wanaosomea fani mbalimbali katika Chuo Kikuu cha Harvard. Si wengi lakini si haba.
Mimi na Dkt. Salim Ahmed Salim tumetoka mbali. Pia tuna kumbukumbu nyingi za pamoja. Naungana nae kusherehekea anapoadhimisha miaka 80 ya kuzaliwa kwake leo. Ameishi miaka mingi, maisha mengi na ametugusa wengi.
#DearDrSalim
Nimepokea kwa huzuni kubwa taarifa ya vifo vya wenzetu 4 wa UDSM. Ni msiba mkubwa sana kwa Chuo, kwangu na kwa familia za marehemu.Nilitamani sana kuwepo pamoja nanyi katika kipindi hiki kigumu. Natoa salaam za rambirambi kwa Jumuiya ya UDSM na familia za marehemu.
Kwa heri Kinana. Hongera kwa kazi nzuri. Daima tutakukumbuka. Hongera Bashiru. Nakutakia kila la heri. Hongera
@ccm_tanzania
, hongera Mwenyekiti
@MagufuliJP
Umoja ni Ushindi, Kidumu Chama Cha Mapinduzi !
Hongera
@SuluhuSamia
kwa kusherehekea kumbukizi ya siku yako ya kuzaliwa. Tunakuombea kwa Mola akujalie umri mrefu wenye furaha, afya njema, baraka na mafanikio tele. Tunakuombea ndoto zako kwa nchi yetu, kwako binafsi na familia yako zitimie. Hongera kwa kazi kubwa na nzuri…
Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Ndugu Abbas Kandoro. Nimemfahamu marehemu Kandoro kwa karibu. Alinisaidia sana katika nafasi ya Mkuu wa Mkoa katika mikoa niliyomteua. Natoa pole kwa familia ya marehemu na kumuombea kwa Mwenyezi Mungu ampumzishe mahala pema
Nikiwa njiani kutokea Iringa kurudi Dar es Salaam nimekutana na watoto katika kijiji cha Mangae mkoani Morogoro. Nimefarijika kuwa wote wako shule. Ni matokeo ya elimu bure. Nampongeza Rais
@MagufuliJP
kwa kuwezesha watoto hawa kuwa shule.
I write to express my deepest condolences to you
@MoiGideon
and your esteemed family, on the passing of your father President Daniel Arap Moi.
We empathize with you and I would like to let you know that we are together with you in mourning.
Namshukuru Mwenyezi Mungu leo nimeweza kushiriki ibada ya Umrah katika Nyumba Tukufu ya Makkah na baadaye kuungana na waumini wenzangu wanaotekeleza Ibada ya Hijjah katika tukio muhimu la kisimamo cha Arafa, kwa dua na kumdhukuru Mwenyezi Mungu.
Nimesikitishwa na kustushwa na taarifa za kifo cha Mwanahabari Athumani Hamisi. Natoa pole zangu kwa familia ya Marehemu na kwa wanahabari wote kwa kuondokewa na mpendwa wao. Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahala pema, peponi.
Today, I start my term as Board Chair of the Global Partnership for Education. Follow my work at
@GPEChair
and
@GPforEducation
. A special thank you to
@JuliaGillard
for her leadership as Chair of GPE over the past seven years.