#HK
is a Member of Parliament for Nzega Rural. Former Minister for Natural Resources and Tourism. Former Deputy Minister for Health. Former Chair, TAMISEMI.
Leo nayo ni siku nyingine. Naishia hapa. Wanasimba wenzangu niliowakera mnisamehe. Wanayanga mnaoshabikia, hayawahusu. Wanasimba mlionipongeza kwa kuhoji tuko pamoja sana. Simba ni yetu sote na tutahoji tu. Hatutokuwa wanyonge kwa sababu hatuna pesa. Hapana. Hatutokubali.
Unakuja inbox kuniambia eti utajitoa Simba, kwani ulipoamua kuingia uliniomba ushauri? Kila ukipata presha kidogo unatishia kujitoa, ndiyo nini? Lipa bn 20 za Simba na weka mambo sawa! Ulaghai wa kutumia pesa una mipaka yake! Usitumie pesa kutunyanyasa na kutufumba midomo.
Kuna watu wanadhani na-post vitu visivyo vya hadhi yangu. Mosi; account ni yangu binafsi, hivyo sipangiwi. Pili, watu wengi huwa hawana muda wa kufuatilia mambo serious ama ya kiingereza. Tatu, mimi siyo mnoko. Mimi ni mwana tu. Cheo kipo leo, kesho hakipo, wana wapo siku zote!
Nimeambiwa kuna msanii wa vichekesho anatafutwa na polisi, akikamatwa mniambie, nitajitolea mwanasheria wa kwenda kumuwekea dhamana na kumtetea. Rais wetu ni mtu wa watu na imejidhihirisha kwa jinsi wananchi walivyojitolea kumuombea dua siku ya kuzaliwa kwake! Wameonesha upendo
It’s ok! It’s ok! It’s ok, very ok kwa Pierre Liquid kufanya anachofanya na kufurahisha wanaoona ‘anachekesha’. Nchi haiwezi kujengwa na watu wanaofanya mambo magumu magumu pekee. Kila mmoja wetu anafanya sehemu yake. Pierre ni mtu huru kwenye nchi yake. Atabaki juu kileleni!
Hili behewa moja (tena used) limenunuliwa kwa sh ngapi? Tumeambiwa yapo haya mabehewa 54, yamenunuliwa kwa us$ 59mn. Kwa hiyo behewa moja ni us$ 1,092,592 ambayo ni sawa na 2.57bn! Hivi hizi ni taarifa za kweli ama? Yamekuja 14 ya awali, bado 45. Kwa nini wametununulia used? 😩
Madenge, if you are in Dar, I would like to invite you to a barbecue, or if not, we can grab a coffee one of these days before I head for campaigns in Nzega rural! 🙏🏿
Watu wengi sana wanaongozwa na uoga, unafiki na ubinafsi kwenye maisha haya. Kwenye maisha yako, kuwa makini sana na watu unaowaita rafiki zako, hao ndiyo anguko lako kuu. Ishi maisha ya uadilifu, uaminifu, upendo na principle, heshima yako itadumu katika hali zote.
#NjeYaBox
#HK
Nikipima kutokana na comments za kwenye page yangu toka jana, viongozi ni lazima tujenge uhalali juu ya kila uamuzi tunaochukua. Maamuzi tunayopigia kura ya ‘Ndiyo’ bungeni ni lazima yawe ‘reasonable’ na sababu zake ziwe ‘fair na zinazokubalika!
#HK
Mara paaap! Nabii Lema is back in Arusha…sipati picha hiyo derby yake na Gambo! 😀🤛🏾 Marathon ya mikutano ya hadhara ya miaka mitatu damn! Wapwa muanze kutuchangia afu tatu tatu za sound system na mafuta ya lorry za matangazo! Kazi inaanza sasa!
#HK
#Fighter
#NjeYaBox
ONYO LA MWISHO KWA MNAOMTUMA KIGOGO: iko hivi; ninawajua, na nyie ni rafiki zangu, tuendelee kuheshimiana, ninawaambia najua mambo yenu mengi; msicheze na tope, mtachafua suti zenu sasa hivi! Mnanijua vizuri, sijifichagi, napiganaga wazi wazi! Jipimeni, mnaweza vita na mimi?
#HK
Kazi ya Urais ni ngumu sana. Tulioteuliwa na Mhe. Rais kumsaidia utendaji/usimamizi wa maeneo mbalimbali hatupaswi kumuongezea Rais frustrations nyingine zaidi. Sisi kwenye Wizara yetu, baada ya kikao na Chief Secretary tulimaliza tofauti zilizokuwepo na sasa hali ni shwari!
Ni wale tu wanaojua ‘marketing’ ndiyo wataelewa anachokifanya
@HajiManara
. Kiufupi, the dude is simply a marketing and promotion genius in his own right! No one like Haji in Tanzanian soccer. He is a living legend that our grandchildren shall read about him.
#HK
#NjeYaBox
Bodi ya Simba ina platform yake, waambie wafafanue suala la uwekezaji. Siyo kunitaka nitafute interview zako za WasafiFM. Muhimu sema tu ‘umelipa 20 bilioni ama la?’ Ningekuwa nimekuomba rushwa ama msaada ningeona aibu, lakini kukopa, kila mtu huwa anakopa, hata wewe una mikopo!
Mwisho wa siku nimesema niliyosema, tena hadharani. Uzuri wa ukweli hua haubadiliki, hata uucheleweshe namna gani, utabaki kuwa ukweli. Naishia hapa. Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Simba na wanachama wengi wameshukuru kwa mimi kujitokeza kuhoji. Wameniomba niachie hapa. Nimesikia
Haya wapwa imetosha sasa! Tuendelee na mengine…maana hasira zenu zote za tozo mmenishushia mimi dah! 🙏🏿🤛🏾😩Mnisamehe nilipowakwaza, najua mambo magumu mno site, ila magari siyo ‘unnecessary cost’, ongeleeni nyingine, zipo nyingi na kubwa kuliko hii ya magari, tujadili hizo!
Hivi kweli Wabongo wote tumeshindwa kuendesha biashara ya DART mpaka tumpe hii kazi kampuni ya nje, au kuna nini? Aibu yetu wallah! Yaani tumekopa, tumejenga halafu kuendesha ma-bus tu na kukusanya hela tumeshindwa! Sasa tutaweza biashara gani?
#HK
Mwanaume hauombi ombi hela ya kula, unaomba KAZI ama mchongo wa deal za hela. Ukikwama sana MWANAUME unaenda kuomba MKOPO kwa wenzako! Huyu ndiye mwanaume tunayetaka kumjenga hapa nchini. Mtanisamehe, I am this tough! 🤛🏾💪🏾. Hata mimi huwa napitia changamoto, lakini NAKOPA! 💪🏾
Binafsi, nimetimiza wajibu wangu kama Raia mwema na kama mwanaCCM mahiri. Kwamba, mama hahusiki kwenye mchakato wa tenda, Wasaidizi wake wasijifiche kwenye kivuli cha Mama, wajibu hoja za umma. Pili, maswali ya umma yako wazi, yajibiwe. Kama hauna jibu utulie. Naishia hapa.
Kuna siku ukweli utadhihiri na maneno yangu yatakumbukwa. Nililazimika kuhoji kwa sababu nilikuwepo toka mchakato unaanza, na nilishirikishwa kama mgeni rasmi, lakini yaliyoazimiwa na kukubaliwa na wanachama wa Simba hayajatekelezwa, leo miaka mitatu. Kuna siku wataamka.
Baada ya kuweka sawa suala la mkopo wa pikipiki, Sasa
@moodewji
nakusubiri ujibu Hoja zangu za msingi, uache kulia lia na kuhamisha mjadala. Ulipaswa kulipa bilioni 20 mwezi mmoja baada ya kupewa offer letter ya kununua hisa za Simba. Umelipa? Ulilipa 10% ya kishika uchumba?
So preposterous! Nimefika hapa airport nakuta hawa jamaa. Yaani watu wameshinda tu kwenye ‘tournament of losers’, wanatuchelewesha watu kwenye vikao vyetu! Sijui wangekuwa kule tulipo sisi wangefanyaje! Kah! 😀🤛🏾
For boys (na Labda wasichana pia wanahitaji kusikia haya! 🤷🏾♂️):
1. Hakikisha unaoa. Kuoa ni lazima. Kuoa siyo lazima uwe na pesa. Ukikua kiasi cha kuzalisha mwanamke, oa! Mengine yatajipanga. Uoe nani sasa, sikia mtazamo wangu!
2. Oa tu mwanamke kama unampenda na una nia ya…
Haya ndiyo mawe makubwa zaidi ya Tanzanite duniani; yamevunja rekodi ya jiwe lililochimbwa na Tanzanite One Mwaka 2005 na kuuzwa nchini Thailand ambako linatumika kama kivutio cha Utalii. Tutazungumza ndani ya Serikali kuona uwezekano wa kuyafanya mawe haya kivutio cha utalii.
Ukimpenda mtu mwambie; Usipepese macho. Asipokuelewa, muoneshe kwa vitendo. Asipokuelewa, achana naye. Hastahili kupendwa. Duniani watu hupenda wasipopendwa. Ila ukibahatika kupendwa, shukuru na changamkia fursa! Maana utajapenda usipopendwa!
#NjeYaBox
I have fallen in great love with mum’s dress code. It’s super smart, respectful and properly done. She has that proper Islamic attire look, neat and meticulous, and very chic. It’s high time for other ladies to imitate 😀.
#HK
Kuna watu wanaamini Mungu sana, na Kuna wanaoamini Mungu na Sayansi na Kuna wanaoamini sayansi peke yake bila Mungu. Kwa sisi tunaoamini Mungu so strongly tunajua, kwa kuwa RAIS wetu ametuongoza huko, kwa Mungu kwanza na sayansi ndani yake, Mungu hatotuangusha. Hatutofedheheka!
Tatizo shangazi umekulia kwenye manukato ya karafuu na mdalasini, kisha Channel na Estée Lauder n.k. Hivyo hukupata fursa ya kujifunza kuwa harufu ya kijasho is actually sexy, ina mvuto na utamu wake! Hiyo utapata kwa Mkulungwa mmoja tu aitwaye Hamisi! 😀
Hamisi, hata ungekuwa mwanaume wa mwisho duniani nisingekubali kuolewa na mtu DEODORANT hajui kutumia; Hebu shika adabu zaku na jifunze kutumia akili badala maumbile mengine! Ulivyokuwa MJINGA hata huelewi kwamba hayo maneno yanamdhalilisha MKEO na WATOTO wako! Ijumaa Kareem
Ulivyo hauna ethics za biashara mtu anakukopa ‘private’, unabanwa kwa hoja unatumia ‘ad hominem’ kukwepesha kwa kumtangaza. Unataka na mimi sasa niseme mambo yako binafsi hadharani? Ama watu/benki waliokukopesha nao wakutangaze? Sema ‘su’ uone!
Report from the lunch rendezvous with Madenge
@rollymsouth
. He is quite an amazing Mpwa!!! We are having a great time. We shall arrange something, some other day, with
@Mangiwakwanza
in Arusha or Moshi!
Ukitaka kuwekeza, anza kujifunza ku-save kidogo ulichonacho. Pili, nunua shamba kwa bei nafuu, pimisha halmashauri na pata hati yako. Tatu, jenga ‘property’ (godown, nyumba etc). Nne, kuwa na wazo kubwa la biashara, ingia benki chukua mkopo kwa dhamana ya jengo lako.
#NjeYaBox
#DearNyerere
, nikiwa Waziri nilianzisha movement ya kukumbuka birthday yako, tukaandaa Tamasha la kumbukumbu ya kuzaliwa kwako. Wapwa wananisulubu kwa makosa ya wasaidizi wangu, hawaoni nia yetu! Ila kiukweli nilipolikagua kwa ukaribu ni wewe mtupu sema kwa picha linabadilika!
Hata mchumba wako, siyo eti anakupenda saana! Acha utoto, amka and man up 💪🏾. Yuko na wewe kwa sababu kuna kitu anapata kwako, wewe ni mission yake, siyo kwamba eti anakupenda saana! Usijidanganye. Simama, kajipiganie! Tosha kwa leo wapwa wa Jamhuri ya Fighters! 💪🏾
#HK
#NjeYaBox
🤔 Hii cheki ni ya benki gani!????
🤔 Hii cheki ni ya tarehe gani???
🤔 Hii cheki ya account gani...???
🤔 Hii cheki namba ngapi ???
🤔Hizi pesa ziko wapi? Zinatumikaje? Transformation imekaaje?
Nikiuliza nitaambiwa chuki ya kunyimwa mkopo wa boxer? Haya…myanywe sasa!
#HK
#Maisha_101
: Kwenye mchezo wa masumbwi, ukimpiga mtu ngumi nzito akaanguka chini huruhusiwi kumfuata na mashambulizi mengine akiwa pale chini. Na hii nayo ni wiki nyingine.
#NjeYaBox
#HK
Boxing Day nzuri kwa Uto. Naungana nao kuwa ‘No Feisal, No Problem!’ Waachane naye tu sasa aende, wako vizuri mno bila yeye! 😀Utani kando, dogo kwa kauli hizi hatocheza Uto kwa furaha na nguvu kama awali, atapotea! Wamuache aufuate moyo wake apate furaha na maisha! Please Uto 🙏🏿
Huyu ndiye Rais wangu JPM ninayemjua mimi! He would like to be funny sometimes...ni mwenye huruma, upendo, mcheshi, hanaga unafiki na ukiwa na matatizo ni ‘baba’ mzazi kweli kweli. Labda kama mimi nimefeli somo la kumsoma vizuri!
#TanzaniaUnforgettable
Niseme nisiseme? Acha niseme tu! Mangungu, Try Again na wengine hawana shida kabisa…Glazer ni tapeli, janja janja, fitna na bahili kweli kweli! Siyo kama Ghalib ama Yusuf, wale wamenyooka, wanatupia mzigo wa Maana kwenye timu! Sisi mpaka leo Glazer hajalipia hisa zake…I repeat…
Leo ninatimiza miaka 43 toka nizaliwe. Ahimidiwe Allah aliye Mkuu kuwa bado Nipo hai mpaka sasa. Najua ni kwa utashi na kusudio lake. Namshukuru Na nazidi kuomba kwake shufaa, siha na mafanikio tele. Ninawashukuruni nyote kwa dua zenu. Tudumu kwenye sala ndugu zangu 🙏🏿
Baba na Mama tukielekea kwenye Mkutano Mkuu wa CCM Taifa 2020. Tunaenda kumpa kura zote 100% Rais Na Mwenyekiti wa CCM Dkt. John Pombe Magufuli kuwa mgombea wetu wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwaka huu 2020.
#MkutanoMkuuWaCCMTaifa
#CCM
#Magufuli5Tena
#HapaKaziTu
#HK
Sikiza; uhalisia wa maisha uko hivi: siku zote huwa tunapenda sana tusipopendwa. Na ukitazama kwa umakini sana utagundua na sisi wanaotupenda kwa dhati kabisa pengine hatuwaoni, hatuwapendi, ama hatuwajui, ama tunawapuuza! Tunawakimbiza na kuwang’ang’ania wasiotupenda.
#NjeYaBox
Huyo
@kigogo2014
na wewe
@MariaSTsehai
ni cowards. Kigogo ameni-block kwa nini sasa? Na wewe sema ‘Suu’ Kama unajiamini Kweli uone ninachofanya hapa! Huna heshima yoyote ile Kwa yale mambo yako unayofanya...
Nimelazimika kujibu kwa sababu ya kulinda ‘reputation’ yangu. Unajua kuamka asbh na kuambiwa umekula 2.58bn ya serikali siyo jambo dogo. Nimefafanua kwa kiwango cha kutosha. Aliyeelewa ameelewa. Ambaye hajaelewa basi akung’ute miguu akalale. Case closed.
Kwanza mimi siyo mwizi, siibagi, na sichukuagi rushwa. Kwenye maeneo ambayo mtu yeyote anayenitafuta kuniharibia hadhi na heshima yangu kama kiongozi msafi huwa mara zote anakwama ni hapo kwenye tamaa ya pesa ya umma. Huwa sina. Hivyo hii vita ni rahisi sana kwangu!
Kuna jamaa wa gazeti fulani wanaotumiwa na watesi wangu, waliwahi kumuandama Waziri fulani wa Maliasili na Utalii huko siku za nyuma mpaka akawapa hela ndiyo wakaacha, wakaanza kumsifia. Mimi siyo mtu wa aina hiyo!
#HK
MNEC amemaliza kazi yake juu ya Zanzibar! 🙏🏿🙏🏿🙏🏿. Hongera sana ndugu yangu, komredi, kaka mkubwa, rafiki yangu Dkt. Hussein Mwinyi. Ushindi wako ni funzo kubwa sana kwetu wanasiasa...
Twita imevamiwa. Leo nimepost picha ile ile Twita, IG na FB nikiwa na binti yangu. Comments za IG ni za kistaarabu zaidi ya za Twita, Mtandao ambao zamani tuliamini umejaa wasomi, watu wazima wenye kujielewa, tukiamini FB na IG ni za millennials. Kumbe vinginevyo siku hizi!
#HK
Naona kwenye comments mnaanza kushughulika na “Kigwangalla”, mimi ni mwanasiasa, Mbunge, jukumu langu ni kusema na kuibua hoja/mijadala, na kutoa ushauri kwa serikali na kwa jamii. Hapa nipo kazini. Napaza sauti yangu! Achana na mimi, jadili hoja, kama huwezi, hiyo shida yako!
Nimepokea taarifa za msiba wa Mzee Benjamin William Mkapa (Rais wa Tanzania 1995 - 2005) kwa masikitiko makubwa sana. Natuma salamu zangu za pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na watanzania wenzangu wote. Pumzika kwa amani baba yetu! 😭😭😭
Mke wangu alikuja kunipa support wiki yote hii nikijiandaa kuwasilisha na kutetea bajeti ya Wizara yetu. Miaka yote amekuwa akifanya hivyo. Ahsante sana mke wangu. Nakupenda.
#Family
#Kigwangallas
#HK
Kuna vijana wakipewa madaraka ama wakitajirika basi hubadilisha tembea/sema yao, dharau inatamalaki na hata husahau walikotoka. Katika maisha yangu mafupi kwenye siasa za kitaifa nimewashuhudia wengine hata wakijiona wakubwa kuliko wakubwa zao. Nawasihi wajifunze kwa Luqman!
Aidha, nimefurahishwa na kauli ya
@kigogo2014
kuwa na kule upande wa pili amewahama. Kwa hili namkaribisha tumuunge mkono Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye mission ya kuchagua Rais Mwanamke 2025. Mimi pamoja na kuwa MWANAUME, nawaunga mkono wanawake Kwa nguvu zangu zote!
Askofu Gwajima afanye uungwana azitafute makala za kisayansi asome kwa kina juu ya chanjo; na kama ana mashaka na sayansi yake atafute wataalamu wampe shule ya chanjo. Hata mimi Mbunge mwenzake nimesoma soma kidogo, niko tayari kumfafanulia maeneo kadhaa na kumuondoa shaka!
#HK
Hawa jamaa ni majangili wa nyamapori, tumewakamata eneo la Loliondo wameua Twiga! Wallah, roho imeniuma sana. Tuko hatua za mwisho kukamilisha Kanuni na taratibu za kuanza kuuza nyamapori kwenye mabucha maalum ili wanaopenda waipate huko, pengine hawa wahalifu watapoteza soko.
FACT: shape ya nyoka/samaki ya treni za EMU (Electric Multiple Unit) na Maglev (Magnetic Levitation) inaifanya isipate resistance kubwa ya hewa na iwe na spidi kubwa na mwisho iende masafa marefu. Mfano ni ile Shinkansen line ya Japan - Tokaido, urefu wa zaidi ya Km 500!
Huyu mzee alinifungulia mlango wa kuingia kwenye game! 🙏🏿🙏🏿🙏🏿. I am so grateful for his life, and I pray he lives many more years to come, happily, and even more successfully.
#HK
#LongLiveMjomba
🤲🏿
I lose sleep for these guys. Sheila and Hawa Kigwangalla rocking their village land for two months now, thanks to Corona! 🙏🏿🙏🏿🙏🏿 😀
#Kigwangallas
#Family
#Alhamdulillah
Thank you
@BraydonBent
. As a Minister of Tanzanian Tourism, I would like to welcome you to Tanzania, at our cost, and to appoint you our goodwill ambassador; if you accept the offer, we will appreciate if you would kindly contact me personally.
#TanzaniaUnforgettable
Wenye uwezo wa kusoma na kuelewa, Someni hapa. Kwa mujibu wa hiki kifungu cha ‘tender document’ hii, muwekezaji alipaswa kuwa na dhamana ya 10% ya amount yote, na ndani ya mwezi mmoja awe amemaliza kiasi kilichobaki. Leo ni miaka mingapi toka atangazwe kuwa mshindi?
#NguvuMoja
Jifunze sana kuwa mnyenyekevu, haswa kama umekuwa maarufu, tajiri ama una cheo. Hizi sifa zisikufanye ufikiri kuwa hauhitaji watu kwenye maisha yako. Unaweza ukampoteza mtu wa muhimu na unayemhitaji sana kwenye maisha yako kwa sababu ya jeuri, kiburi na kujiona.
#NjeYaBox
Bodi ya Simba inapaswa kutusaidia kujua ni lini hisa za Simba 50% zililipiwa? Na kama hazijalipiwa, zitalipiwa lini? Na ni nini kinampa mamlaka Mo (ambaye hajalipia 50% yake kwa 20bn alizoahidi kulipa) kuwa Mwenyekiti wa Bodi? Kama Bodi haina majibu haya wajiuzulu tu!
#NguvuMoja
Kuna ujanja na Kuna ujanja ujanja. Ujanja ni pale
@SimbaSCTanzania
tulipokubali kuhama kutoka kuwa Klabu ya Wanachama na kuwa Kampuni. Ujanja ujanja ni hiki kinachoendelea sasa hivi; hisa hazijalipiwa. PA wa mwekezaji ambaye hajalipia shares anateuliwa kuwa CEO!
#NguvuMoja
#HK
Katiba ya Marekani imerekebishwa mara 27, na imedumu toka Mwaka 1789, zaidi ya miaka 230, na bado Kuna kero na changamoto kwenye maisha ya watu. Majirani zetu kadhaa wameandika katiba mpya na bado kuna kero/changamoto na wengine wanajuta kubadili Katiba zao. Katiba isubiri!