THREAD: Makosa ya kuepuka unapoandika proposal, concept note au expression of interest. Wengi wetu wenye taasisi, asasi au kampuni inatulazimu kuandika proposal au concept note kuweza kupata fedha kama mtaji au kuendesha miradi au strategic partnerships;
Sio sifa wanafunzi wako wakifeli. Nikiwa first year UDSM Sheria, kuna lecturer alituambia kabisa hata nusu hamtograduate. Hii ya kukamia watu kufeli ili kuonesha unguli wa tasnia fulani umepitwa na wakati.
Huku mtaani GPA sio kigezo pekee cha mafanikio. Wala ulichosomea :(
No, my husband was not trying to cross the border into Kenya. He didn’t need a passport to be at Namanga for his personal business, Tanzania’s side, broad daylight. We live in Arusha for God’s sake. The apprehension didn’t happen yesterday as reported, it was Friday last week.
Nimekaa kwa kutulia nimewatafakari hawa wadada. Kwa bahati mbaya au nzuri, tunachokiona ni matokeo ya mwanaume waliye naye. It may not be popular opinion, ila wanawake tunatengenezeka kirahisi sana...kuwa vibaya au kuwa vizuri. Wabarikiwe
Nitayainua macho yangu, nitazame milima. Msaada wangu utatoka wapi? Msaada wangu u katika Bwana, aliyezifanya mbingu na nchi - Zaburi 121 kwa ajili ya mume wangu
@LazaroNyalandu
Je wajua? Nilikuwa wa kwanza katika somo la Historia nchi nzima katika mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita mwaka 2004. How? Nilisoma vitabu kuliko ‘notes’
@ElimikaWikiendi
#HumbleBrag
😀
#THREAD
Umemaliza Chuo? Uko in between ajira/kujiajiri na kumaliza Chuo? Huna Cheti cha Elimu ya Chuo na umejiajiri au umeajiriwa? Cheti sio kila kitu. Uzi huu ni wa ujuzi mbalimbali utakaokutofautisha au kukuongezea ufanisi kufikia malengo yako. Elimu sio kigezo ingawa ni msingi
I appreciate everyone who got in touch to check on me and kids. Including cadres of main and opposition political parties. There is pain, we all need to heal. I have no energy to be angry. I hope we find peace, unity and compassion as a nation. May God bless our country Tanzania
Struggling to make a decision about something usually means there are other smaller decisions to be considered before getting to the actual big decision. Trust the process
My husband is back. Praise, Glory and Honor to God. Asanteni sana kwa upendo wenu. Hakika yanayotuunganisha ni mengi na muhimu kuliko yanayoweza kutugawanyisha. Nawapenda wote, nawashukuru wote. WOTE. Naendelea…
Wanaobet wala sio vijana peke yao. Leo nimekaa pembeni ya baba mmoja tukisubiri huduma aliniomba nimchagulie ‘mechi’ akihisi nina bahati kwahiyo anaweza kushinda. Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuona vinavyochezwa. Aliniambia hajui jinsi ya kuacha kubet
Ushauri wa zamani: Ukienda kwenye hafla, ni bora ukae viti vya nyuma kuliko kukaa high table, kama ni wa kukaa high table utafuatwa huko nyuma upelekwe mbele
Tafsiri ya sasa: Usijipe umuhimu
THREAD: Kwanini Shule za Masista zina rekodi nzuri ya ufaulu kuliko Shule nyingine. Naelezea uzoefu wangu binafsi baada ya kusoma Shule mbili za masista, St. Francis (Mbeya) na St Mary’s Mazinde (Tanga), nikiwa miongoni tuliopata Division One enzi hizo...
Hii ni habari njema kwa Elimu yetu. Motisha ya kukaririsha watoto na kuwafundisha masaa 12 ili Shule iwe kumi bora sasa hakuna.
Tuendelee kujenga misingi ya ufundishaji bora kwa lengo la kukuza uelewa, turudi kwenye mantiki nzima ya mtu kwenda shule.
Elimu bora sio bora Elimu!
Tuna kazi kubwa sana na wadogo zangu wa kike na wa kiume hasa zama hizi za mitandao. Tulikuwa na mila nzuri sana za kuwafundisha wavulana kuwa wanaume wanaojitambua na kujua nafasi yao kwenye maisha ya mwanamke. Siku hizi watu tupo tupo tu, si imani si mila :(
Kuna interview mtu aliulizwa mshahara anaotarajia iwapo atapata kazi. Akataja nusu ya pesa iliyopangwa kama mshahara.
Muajiri wake akafurahi kuona wanampata kwa nusu gharama.
Tulitetea sana alipwe kilichopangwa na sio kumlalia kisa ufahamu mdogo wa thamani yake au shida ya kazi
Usichague kazi kwasababu hujaisomea au hauna ‘passion’ nayo.
Utafanyia kazi ‘passion’ yako kwa ufanisi zaidi ukiwa na uhakika wa kula.
Tofautisha ulazima na hiari.
Je wajua? Kuwahi kumuanzisha mtoto chekechea hakumjengei tabia za kujifunza. Bora abaki nyumbani awe mbunifu na mdadisi bila mipaka inayowekwa shuleni
@ElimikaWikiendi
Natumai sote tumejifunza kuwa na ubishi hoja na sio ubishi hewa. Kilichofurahisha kati ya shangazi na mheshimiwa ni uzito wa hoja za kila mmoja, ndio ligi ikanoga. Wale wenzangu na mimi wa kupinga alimradi tu upepo uko kusi na sisi tuko kasi, chai za hyatt tutazisikia timeline 😂
Asanteni kwa kushiriki nami kwenye
@ElimikaWikiendi
.
#Bonus
Je Wajua? Inawezekana mwanamke akapenda urembo kama anavyopenda vitabu, akaweza kuongoza kazi za nyumbani kama za ofisini, akaweza kuwa mama kama anavyoweza kuwa kiongozi na akampenda Mungu kuliko anavyoipenda dunia 😃
Naandika hizi threads kwa uzoefu wangu binafsi. Nimeshajaribu vitu vingi. Ninavyoandika hapa ni vile ambavyo vilinisogeza hatua nyingine. Kila siku nataka nifanikiwe zaidi. Kila siku najifunza. I hope you feel the same way. Let’s grow together!
Ingekuwaje binadamu tungekuwa tunawaza kwa sauti? Kuna ya moyoni yanayobaki moyoni. Si kila kisemwacho kimekamilika, kuna yanayobakizwa, hayatotamkwa kwa maneno ila utayajua kwa vitendo
Do not escape your shortcomings by always finding somebody else to blame. There will always be shortcomings and people to blame, but are you getting better?
Ukiwa unaanza, anza na hali halisi. Usianze na vile ungependa vitu viwe. Pambana vitimie. Work with what you have in front of you. Things are as they are. Work your way up
THREAD: Mambo ya kuzingatia unapoanza kufanyia kazi wazo lako kuwa biashara au taasisi. Hizi ni hatua za awali kabla ya kuanza usajili na taratibu nyingine za kisheria
Alafu baba ni baba na mama ni mama. Let’s not normalize mothers taking on fathers’ roles and disregard fathers.
Baba wawe baba. Mama wawe mama.
Labda tu iwapo mapenzi ya Mungu yamefanya vinginevyo.
Tunahitajiana.
Jaribu kuwa consistent uone itakuwaje. Moja ya vitu ninavyoamini vinatofautisha kufanikiwa na kutokufanikiwa.
Shikana na jambo lako kwenye milima na mabonde mpaka uone mwisho wake.
Kwahiyo habari yangu ikiandikwa Nyalandu na haimhusu mume wangu ni kosa? Ikiandikwa Kotta na hainihusu mimi, inamhusu baba yangu, ni kosa? Tatizo ni identity au identification? Hii kanuni ni habari ikiwa mbaya tu au na nzuri pia? Poleni sana
@kwanza_tv
THREAD: Ninavyoweza na ninavyotamani kuweza ili kuongea vizuri kwenye hadhara. Topic ni public speaking, kwa inaotuhusu, hii huwa ni nafasi ya kujinadi (yes you, people buy from people), kunadi biashara/huduma yako na kualika wadau/partners wa kushirikiana nao kwa gharama nafuu;
So proud of my former school, St. Francis Girls Sec. School for ranking top at the Secondary School National Exams. Qualified teachers, discipline, enabled self learning, cultivating self motivation and Faith got them there. It’s possible to have every student score Division One!
THREAD Jinsi ya kumudu NETWORKING kama sehemu ya mafanikio binafsi na ya biashara yako. Nimekosa tafsiri ya moja kwa moja lakini kuna haja ya kujua jinsi ya kujichanganya na kuwasiliana na watu, hasa sehemu za makutano au dhifa mbalimbali
Congratulations lady
@bvrbvra
- I believe in your capacity and ability to lead Simba Sports Club to newer heights. Godspeed in all your plans, you got this!
1. Jifunze ku-network. Usikae ndani. Jifunze kuongea na watu, kuwasikiliza na kuwa na maswali sahihi ya kuwauliza. Jitahidi kukuza ufahamu wako wa mambo mbalimbali ili uwe an interesting and interested person, ufahamu unakuzwa kwa content unazo-consume kila siku...
THREAD Uandishi wa email unaoweza kuleta matokeo chanya. Kwenye ulimwengu wa leo, mawasiliano ya kielektroniki imekuwa ni muhimu na lazima. Kuanzia Covid iliyopita na hata hii ya ajabu ajabu, emails na ‘zoom’ zimechukua nafasi ya makutano ya ana kwa ana kwa wengi wetu makazini;
Lots of birthday love to our daughter, Sarah Divine Nyalandu. She is the first person to call me mama. Happy 12th Birthday Tutti Frutti, May our Lord Jesus Christ shine His Light today and always!
Not everyone learns through struggle.
What doesn’t kill you, may not necessarily make you stronger.
You may become weaker.
Let’s not glorify hardships.
It’s okay to ask for help 🙏🏾
Kila unapoweza kuthubutu, usiache kujaribu. Itambue hofu lakini usikubali ikuendeshe. Ulichoazimia kufanikisha kikupe nguvu kuliko mashaka uliyonayo. Nakutakia wiki njema