Author 6 Books AMAZON 📚📚=| MBA | MLUMBI I Leadership Expert /John 15:16 IMC | Trainer-0757464874 MD:AYLF and PLO Lumumba Foundation SUB YOUTUBE —Joramu Nkumbi
Siku Saba Zilizopita
1.Leo
2.Jana
3.Juzi
4.Majuzi
5.Juzijuzi
6.Majuzi yale
7.Kijomba.
Siku Saba Zijazo
1.Leo
2.Kesho
3.Keshokutwa
4.Mtondo
5.Mtondogoo
6.Kitondo
7. Kitondojogoo au (kitojo)
Ni kicheko taanusi mhadhiri
anapopata sabatiko, ni kicheko
bojobojo mwana anapoona titi la
nina, ni kicheko tumbitumbi baharia
anapopata halasa, ni kicheko
belele mkulima anapopata
mtamba na liweya, ni kicheko biwibiwi biharusi anapopata ukonavi, wewe kijulanga unachekea nini?
Uzimbezimbe na uzohali mshahara wake ni ukata, msaragambo na mtulinga malipo yake ni ukwasi, magamaga na kuwa fumbwe mshahara wake ni sekeneko, Usalata na ufyosi malipo yake ni gunia la aibu na fedheha. Bali jamala na insafu malipo yake paradiso. Ewe mja nadhari njia ya peponi
Janja janjaruka, wakahambarara
walipoulizwa wakaona kimuyemuye.
Wakajaribu kupiga mafamba na kunyenga kwa nyama ya ulimi ila hawakufanikiwa kwa busara za wanakijiji. Hatimaye wakatema cheche kandokando ya balasi la petroli ndiposa amani ikatoweshwa, nayeyuka.
Nipo Katika Chuo Kikuu cha Syracuse mahali ambapo Rais wa Marekani JOE BIDEN alipata Shahada yake ya Sheria. Na Katika chuo hiki ndipo alipompata mkewe Neilia Hunter na kumuoa.
Mimi mja chochole nilipokutana na msharafu ONI SIGALLA alinifunulia gombo na kunipa waadhi nishikilie kidinindi, ama kwa hakika maneno ya mswahili ni kikoi cha kibiri hayachakai. Ukarimu wake ulinirovya rovurovu kama biskuti ndani ya kiowevu. Akraba yangu shukrani belele nayeyuka
Kwa maneno dhahiri shahiri,Mama amtemea mgogoyo mwanake kigoli. Ewe banati mwenye pambo la bronki na bizimu na tabasamu taanusi chunga maago wana miba nungunungu.Mama
alipomaliza kutema mgogoyo alikema, ayala mwenda pweke ni tijara ya mwindaji.
Msharafu SALIM KIKEKE
@Salym
- ilikuwa ni TAJAMALA kuonana
Ushauri wangu kwa mja, endelea kuwa Upande wa Mola, “MEZA MRUTUTU”dhiki yako ni ya Kitambo, heshimu Wazazi na tambua kwamba mwana mdharau nina atakula MUMBI, mwana mdharau ibada kuzimu enda Kiona. Nayeyuka 🙏
Tu katika biwi la Simanzi;
Mzee Ali M. Kibao tunaomba utusamehe baba. 🙏 Ya Rabi Stara 🙏
Makosa Saba ya Ulimwengu
1. Utajiri bila maadili
2. Raha bila dhamira
3. Maarifa bila tabia
4. Biashara bila uaminifu
5. Sayansi bila utu
6. Ibada bila kujitolea
7. Siasa bila ubinadamu
Ndugu zangu Waswahili, mwenye nguvu mpishe-
Mimi ni kingulima, tena kishirazi, tena kidurusi huwezi nifananisha na mlima Kilimanjaro huko ni kunionea bure bilashi
Mswahili Madebe apewe heshima yake 🙏
Give a man land, give a man a wife, and don't tell him anything; he will stay there forever. I came, I saw, I loved.
To the beautiful people of Rwanda, Africa is one.
Ndugu, kula ugali wako kwa amani, salimia majirani zako kwa furaha, ota jua, kunywa maji ya kutosha, kula embe, chungwa, mabokwe, ama karakara ikiwa una senti, patana na Mola wako, fanya jambo unaweza usinyoshe kidole.
Safisha chumba chako kabla hujasafisha dunia. Nayeyuka 🙏
Leo kwa kudra za JAALIA,kwa kadari yake MOLA nimetembelewa nyumbani na TBC kufahamu zaidi ni nini hasa sababu ya safari hii ya ULUMBI. Kuja kuniona mimi kumenirovya rovurovu na kunitebweresha tebwere,napokea mambo haya kwa kuduwazwa,kwa DUA na SALA.Nayeyuka kwa tafakari za uketo
Amejawa HASANATI, Ingawa yeye ni Mti Mkubwa wenye mizizi na matawi yake kotekote ila ulikuwa radhi kumhifadhi mwana wa nyuni, mwana wa nyuni akapata kivuli japo kwa sekunde. Umejawa hasanati na huo ni uungwana mkubwa, shukrani belele akraba yangu janabi SALIM KIKEKE
@Salym
Msitu bila miche michanga ni Msitu mfu, “Chinua Achebe” aliwahi kuuliza Swali iko wapi miche michanga itakayo chipukia? Baada ya ile migomba mizee kufariki? Dua yetu uwe Salama ndugu yetu hadi utakapoturudia 🙏
Kwa Makadara yake Jaalia nipo ndani ya Ukumbi wa Umoja wa Mataifa. Hapa ndimo Viongozi wa Ulimwengu hukutania.
Hiki ni kiti chetu Watanzania, Kila ikifika Usiku huwa navua mavazi yangu ya kitumwa na kuvaa mavazi yangu ya kidiplomasia.Fikra hii siwezi kunyang’anywa.
IKULU YA MAREKANI
The White House is the official residence and workplace of the president of the US. It is in Washington, D.C, and has been the residence of every U.S. president since John Adams in 1800. The term "White House" is a metonym means president and his advisers.
Ukipata nafasi jaribu kuishi,
Maisha ni hidaya
Maisha ni tajamala
Maisha ni azizi
Je, wewe ni masikini hata ushindwe kununua hewa ?
Uza hofu nunua tumaini
Uza huzuni nunua furaha.
Karadha ya Mshahara = Salary Advance
Malipo ya Ajari = Malipo ya Overtime
Lugha ya Safihi = Lugha Chafu,
Likizo ya Uraufu = Compassionate Leave,
( kwa kufiwa, kuugua)
Tanzu = Tawi
Hiba = Zawadi
Bainifu = Outstanding (sifa njema za
kipekee)
Nimetondoa Utondozi.
Muhtaramu Job Ndugai tulikutana Nairobi Kenya katika tukio la National Prayer Breakfast alialikwa kuwakilisha nchi, nilialikwa kuwakilisha vijana. Katika Mazungumzo aliniambia, “ Usiache kupigania kile unachokiamini, tafuta kuwa bora kuliko jana, kesho yako ina matumaini”
Mwanzo wakati naanza kusoma falsafa,kusudi nijue namna ya kuendesha maisha haya mafupi, nilimsoma Budha,Mahatma,Dr. MLKj, James Alen,Nyerere, Mandela,Wangari,nk. nilivutiwa kiukweli na kuwafanya wanasihi wangu.Nilimposoma Bwana Yesu kuna namna siwezi eleza nimependa falsafa yake.
Ametononoka tena amewanda tangu alipoacha ulanzi, chang’aa na mtukuru, haendi tena kwa majaka, Kazini amerudishwa anakula masurufu marupurupu na mukafaa, Waama nadhari njia ya peponi. Sio kitimbakwiri tena ni yeye na Mola wake, Sako kwa bako na familia yake. Ewe mja sarifu maisha
Bilionea Ali Mufuruki aliwahi kuniambia
Ipo tabia ya wakubwa inayoitwa “hypocritical behaviour - kicking away the ladder"
Kati ya mwaka 1776 na 1940, wanasiasa wengi wa Marekani walikuwa wafuasi wa sera za kulinda masoko na kutokuruhusu wawekezaji kutoka nje.
Kumbe na huku nyumbani SINGIDA wanafuatilia ULUMBI - akraba zangu waliponiona nikipita mtaani wakiwa katika hali ya MTIMBWIRIKO , kwa tamwa tulifurahi kwelikweli
Mzee Mchekeamwezi alipokutana na Mzee Nunaucheke alimwambia umeadimika kama kicheko jehanamu, na kama barafu ya kukaanga, naye akajibiwa nawe umeadimika kama mizizi ya mawe na kama maziwa ya kuku. Wakacheka sana na kupigana pambaja kisha wakaambatana kama mkia na kupe.
Kwa Kudra za Mwenyezi Mungu nilipata nafasi ya kumtembelea Seneta wa jimbo la Arkansas John Boozman. Huyu ni moja wa wanasiasa makini sana katika Taifa la Marekani.
John Boozman is the senior US senator from Arkansas, a seat he has held since 2011
A member of the Republican P.
Maana ya semi nilizozitumia;
Meza Mrututu = Kuvumilia Machungu au Maovu
Kula Mumbi = Pata taabu au Shida
Meza Joto lako = Tuliza hasira yako.
Nina = Mama
Pamwe na Msharafu Balozi wa Tanzania Nchini Ujerumani Dkt Abdallah Possi,
Nimepewa MLAHAKA mwema hapa Ubalozini - Berlin, tumezungumza mazuri kisha nikapata Sharubati ya Zabibu na Udohodoho ulikuwepo mezani. Ndugu hawa wamejawa hasanati na ukarimu furifuri. Shukrani belele.
JITIE MOYO mwanakwetu
Tumia Abra kuongeza UMILISI wako
Tumia Satua kujikwamua kwenye Lindi la unyonge
Penda mvuvumko wa Afrika kwamba unaweza kufanikiwa ukiwa nyumbani
Penda uanamajumui kwamba Afrika ni moja na binadamu wote sawa
Penda kufikiria uko huru, Afrika ni Kanzi.
White House, DC
Mujarabu nilipofika karibu na IKULU ya MAREKANI wimbo wa Taifa la Tanzania ulianza kuimbwa, Moyoni nilifahamu kwamba Mwalimu Nyerere aliwahi kuimbiwa Wimbo huu alipokaribishwa na Mwenyeji wake rais JF Kennedy- Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania 🙏🙏🙏
Baada ya kupoteana miaka na mikaka mujarabu walipoonana walipigana pambaja, kwa furaha riboribo walikumbatiana papatupapatu. Wakakumbushana habari za mchwa na vingulima na habari za kumbikumbi na vidurusi ndiposa wakacheka kochokocho. Ungewaona ungefurahi pia, nayeyuka kihawinde.
Mwanahabari mwenye JAHA na ULUWA
@Salym
. Jina AJUADI, jina jema ni bora kuliko marashi ya marhamu ya nardo, mwisho wa safari hii ni mwanzo wa safari nyingine, Asante kwa kutuonesha namna
mwanahabari bora anapaswa kuwa mfano faafu.
Ulumbi umenipa familia kubwa sana Kila mahali ninapokwenda, Huyu ni Mtanzania mwenzangu Berlin Ujerumani. Amekuja kunisalimu na hili ni Jambo kubwa. Asante Sana kaka
New York City- Times Square
“Learn from yesterday, live for today, hope for tomorrow. The important thing is not to stop questioning.”
“He who can no longer pause to wonder … his eyes are closed.”
“A happy man is too satisfied with the present to dwell too much on the future.”
Sheria njema huwaleta wanadamu karibu na Mola wao. Tena hulinda maskini.
Sheria njema ni Msingi wa Uumbaji.
Sheria imo ndani ya Uumbaji.
Sheria njema ni Gundi inayoshikilia Ulimwengu pamoja.
Kitu cha kwanza ambacho Mungu alimpa Musa kwa ajili ya kujenga taifa ni SHERIA.
Mazungumzo yangu na NGUGI WA THIONG’O
Hii ni kama bahati, Nikiwa British Columbia Profesa Sultan Somjee aliniunganisha na Prof. Ngugi wa Thiong’o nikapata kumsabahi kwa Simu
Waama Mwana mtambaa kule huwakaribia wazee kwa kale. 🙏🙏🙏