Speaker of the National Assembly of Tanzania 2022 - |Deputy Speaker of the National Assembly 2015-2022 |16th Deputy Attorney General of Tanzania |Lawyer
Namuomba Mungu atujalie utajiri wa hekima, busara pamoja na kuwa na moyo mkunjufu kwa kuwa vyeo, mali na majigambo ni vitu vya kupita katika maisha, bali utu wema pamoja na hofu ya Mungu vitadumu milele na kuacha alama isiyofutika katika Maisha yetu ya Duniani.
Katika maisha tumebarikiwa uwezo wa kuona na kujua mambo yaliyo tokea jana na yanayotokea Leo hakuna ajuaye kesho yake itakuwaje, hivyo ishi na watu vizuri, kwa upendo na amani kwasababu hatujui kila mtu tunayekutana nae kesho atakuwa nani? au atakuwa sehemu gani?
Jokate my dear, nafurahi sana kila nikiangalia hatua zako za kuifanya Kisarawe, Pwani, Tanzania sehemu salama na njema kwa wote, hasa watoto wa kike. You rock! Am very proud of you. Go girl, greater heights! No limit, not even the sky
@jokatemwegelo
. Lots of love 💕
Leo kazi yetu Watanzania ni moja tu, kwenda uwanjani kwa wingi kuisapoti timu yetu ya
@simbasctanzania
, ili kuhakikisha inaibuka na ushindi. Do or Die.
#yeswecan
You fought a good fight Mr. President. You led Tanzania with integrity, honesty, commitment and hard work to fulfil your purpose in this world. We will miss you Baba. May the beautiful soul of HE BW Mkapa Rest in Eternal Peace. Amen.
Kila La heri
@simbasctanzania
, wawakilishi pekee wa Tanzania katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika nina imani mtapambana hadi tone la mwisho, YES WE CAN.
Watanzania tulipoungana kwa pamoja katika mashindano ya kuhifadhi QURAN TUKUFU Jijini Dar es Salaam. Hili ni jambo la kipekee sana kuwahi kutokea. Hii ni picha halisi ya amani na upendo.
Siku zote kumbuka kuwa unapolalamika kuwa umefeli katika maisha usisahau kuwa, kuna mwenzako ameshindwa kupata hata hiyo nafasi ya kufeli lakini wewe umefeli kwasababu umepata nafasi ya kujaribu ambayo kuna wengi wameikosa.
#TimizaMalengo2019
Jamii inahitaji kuwa na mtu ambaye anaweza kusimama na kufanya jambo kwa manufaa ya jamii nzima bali sio kwa manufaa yake, jamii inahitaji mtu anayeweza kusimama na kuyatetea maslahi ya wanyonge, mtu anayeweza kuhamasisha na kupigania maendeleo ya jamii.
As we join the Burundians to mourn the passing of HE Pierre Nkurunzinza, we are reminded that life is too short. Live a life that leaves a mark behind, however small. May his soul RIP.
#letlovelead
Una kila sababu ya kuishi kwa furaha na amani, usiumizwe sana na vikwazo au maneno ya watu bali uwe hodari na imara wakati wote ili uweze kutimiza malengo yako.
#tbt
#TuijengeTanzaniaYetu
Hapa Duniani unaweza ukatenda wema mpaka ukakosa nguvu za kwenda zako, hivyo kuwa makini na watu wanao kuzunguka maana moyo wa Mwanadamu ni kiza kinene huwezi kujua yupi ni mkweli na yupi ni muongo katika maisha yako.
Tanzania tumejaliwa kuwa na vivutio pamoja na mazingira mazuri na ya kipekee, nina kila sababu ya kujivunia kuwa Mtanzania kila nitembeapo naona uzuri wako wa asili na wa kuvutia. Daima nitakulinda na kukutunza Tanzania yangu. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika.
Kesho Jiji la Mbeya linaenda kuandika historia kubwa na ya kipekee kwa maana wasanii Wasafi watalisafisha Jiji Letu kwa burudani ya aina yake. Naongeza sauti Wanambeya wenzangu hii si ya kukosa, kwasababu wananchi wote tutaweza kushiriki katika burudani hii bure.
Leo nimepata wasaa wa kuzitembelea familia tano za watoto wenye ulemavu Jijini Mbeya, lakini pia kwa kupitia Taasisi ya Tulia Trust tumeweza kuwapatia msaada wa baiskeli za kutembelea kwa lengo la kuwasaidia watoto hao katika kuwarahisishia shughuli mbalimbali.
Watanzania tupo nyuma yenu tunawaombea usiku na mchana ili muweze kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania. GO TAIFA STARS, GO TANZANIA.
#AFCON2019NIZAMUYETU
Mimi nina imani na
@simbasctanzania
wawakilishi pekee wa Tanzania katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika, Leo pale kwa Mkapa ushindi ni wetu, kwani Simba ikishinda Tanzania inashinda pia.
#yeswecan
Leo nilipata wasaa wa kununua mahitaji mbalimbali ya nyumbani kutoka Sokomatola lililopo Jijini Mbeya lakini kubwa zaidi nimefurahishwa na huduma na ukarimu wa wafanyabiasha wa Soko hilo.
#BlessedTulia
#MindyourBusiness2020
Leo nimepata nafasi ya kuwatembelea ndugu zangu wa Kata ya Iyunga na kusikiliza kero zao hasa suala la kutokulipwa fidia zao kutokana na ardhi yao kutumika na wawekezaji ikiwemo Chuo Cha MUST pamoja na Jiji la Mbeya. Nimeazichukua changamoto hizi na kuahidi kuzishughulikia.
Kamwe usikubali mapungufu na udhaifu wako viwe kikwazo katika kutimiza ndoto zako, kwani hivyo hivyo ulivyo unaweza kufanya mambo makubwa na kuushangaza Ulimwengu cha muhimu ni kujiamini na kuthubutu.
#TimizaMalengo2019
"Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole kiasi ; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria" - Wagalatia 5:22-23.
Nawatakia Jumapili njema na yenye furaha.
Today I will bless the womb that carried you. You are a great man, given to us by God. Blessed be Mama John, blessed be the day you saw the light. Happy Birthday Your Excellency JPM.
#TumekuelewaJPM
#BlessedTulia
Happy Birthday Mr. President, HE. Dr. JPJ Magufuli. May the good Lord protect you. Blessed is the Womb that carried you, one of the greatest sons of Africa. May the soul of Baba John Rest In Peace. May the Almighty bless your mother, May she live long.
@MagufuliJP
Mawazo na mitazamo yetu vina nguvu kubwa katika kubadilisha maisha yetu cha muhimu ni kuishi katika ndoto zetu na kuamini siku moja zitatimia bila kusahau kujituma, kujitoa pamoja na kufanya kazi kwa bidii.
Watanzania tukutane uwanja wa Taifa siku ya Jumamosi, kuwapa hamasa wawakilishi pekee wa Tanzania katika michuano ya Klabu Bingwa Africa
@simbasctanzania
, nguvu yetu mashabiki ndio ushindi wa timu yetu. YES WE CAN.
#ThisisSimba
Hatimaye tumefika katika kilele cha Mlima Kilimanjaro, hiki ndicho kilele kirefu Barani Afrika. Kufika katika kilele hiki ni ishara ya kufikia malengo yetu ya kukusanya shilingi millioni 100 kwa ajili ya kusaidia kupata mashine za kutengenezea taulo za kike.
Ilikuwa sekunde, dakika, saa, siku, wiki, mwezi, na sasa mwaka! Ulifanya yaliyokupasa. Pumzika kwa Amani Ruge the Great! You are always remembered, admired. Your determination unbeatable! RIPower!
@cloudsfmtz1
Natoa pole kwa familia na Wafanyakazi wote wa IPP Tanzania ni wazi tumepata pigo kubwa ila mwenyezi Mungu awasimamie na kuwapa nguvu katika kipindi hiki kigumu. Bwana ametoa na Bwana ametwaa Amen.
#RIPDKTMENGI
Nimefarijika sana kuhudhuria Mashindano ya kuhifadhi QURAN TUKUFU yaliyofanyika Wilayani Kondoa, Dodoma nikiwa pamoja na Dada yangu Dkt. Ashatu Kijaji (Mbunge wa Jimbo la Kondoa). Hakuna jambo linaloleta furaha kama wanajamii kujumuika kwa pamoja katika kumuabudu Mwenyezi Mungu.