Welcome to the leading Radio Station
#AzamUFM
| Part of Azam Media Ltd/Bakhresa Group | 107.3 DSM, 101.7 Dodoma, 96.5 Arusha, 98.7 Shinyanga |
#SisiNiWewe
Wizara ya Afya ikimtaka Mtaalamu wa tiba asili, Masoud Sumini ambaye ni Mkazi wa eneo la Zuzu jijini Dodoma kusajili dawa zake ili zitambulike baada ya kujizolea umaarufu kwa matibabu ya kuunga viungo vya binadamu na mifugo vilivyovunjika bila kugusa mwili wa mgonjwa.
Uongozi na wafanyakazi wa UFM Radio, tunawapongeza wachezaji, benchi la ufundi uongozi na mashabiki wa Yanga kwa kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi kuu 2022/2023.
#SisiNiWewe
#YangaSC
@yangasc1935
Simba SC imetangaza kumsajili Kiungo mkabaji, Fabrice Ngoma raia wa Congo DR akitokea klabu ya Al Hilal ya Sudan kwa mkataba wa miaka miwili.
#UFMUpdates
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally amesema bado klabu hiyo haijamaliza usajili na kwamba inamaliza mazungumzo na nyota wawili watakaocheza eneo la mbele na golini.
#UFMUpdates
#SimbaSC
#Usajili
#UsajiliSimba
GWIJI LA SOKA AFARIKI DUNIA
Mchezaji nyota wa zamani wa Argentina, Diego Armando Maradona amefariki dunia leo Novemba 25, 2020 akiwa na umri wa miaka 60.
Taarifa za kifo cha Gwiji huyo zimethibitishwa na Shirikisho la soka nchini Argentina kupitia kwa Rais wake Claudio Tapia.
Kiongozi Mkuu wa Sokwe huko katika hifadhi ya Taifa ya Mahale iliyopo Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma amejiuzulu uongozi baada ya kupata kashifa ya kumbaka dada yake ...
#UFMUpdates
Kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Saidi Ntibazonkiza aliyesajiliwa katika dirisha dogo la usajili amefanikiwa kupachika mabao matatu na kutoa pasi moja iliyozaa goli katika mchezo uliopigwa leo dhidi ya Tanzania Prisons.
Unauonaje muunganiko wa Chama na Ntibazonkiza?
#UFMUpdates
Kwa mujibu wa mitandao ya kijamii ambayo picha hii imesambaa, imemuonesha Mfaransa aliyesafiri hadi Ivory Coast kumtafuta yaya aliyemtunza miaka 38 iliyopita wakati baba yake akifanya kazi nchini humo kabla ya kuacha kazi na kuhamia Ufaransa..
#UFMUpdates
Klabu ya Simba SC imethibitisha kumsajili golikipa, Ayoub Lakred (28) aliyekuwa akiichezea FAR Rabat ya Morocco inayonolewa na aliyekuwa Kocha Mkuu wa Young Africans, Nasreddine Nabi.
#UFMUpdates
Klabu ya Soka ya Simba imeibua upya matumaini ya kutinga hatua ya robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika
#CAFCL
baada ya mchezo wao wa nne katika hatua ya makundi dhidi ya Wydad Casablanca kumalizika kwa ushidi wa mabao 2-0.
#UFMUpdates
#CAFChampionsLeague
#CAFCL
“Tuweke akiba ya maneno ni nani anakuja katika eneo la mbele, anaweza kuwa Luis Miquissone au mchezaji mwingine mkubwa, ndani ya wiki hii tutakuwa tulishajua …,”
@ahmedally_
kwenye kipindi cha Sports Bando cha hapa 207.3 UFM Radio.
#UFMUpdates
#UsajiliSimba
#LuisMiquissone
Klabu ya Simba SC imesema kuwa imefikia makubaliano ya pande zote mbili ya kuvunja mkataba na Kocha Mkuu wa kikosi cha kwanza, Roberto Oliveira (Robertinho) na kocha wa viungo, Corneille Hategekimana.
“Feisal Salum ni mmoja wa wachezaji bora nchini, watu wanatuhusisha naye na sisi tunapenda pia tunafurahi kusikia tunahusuishwa na Feisal kwa sababu ni tabia ya kila timu kubwa…”
Hashim Ibwe, akielezea tetesi za usajili wa ‘Feitoto’ anayehusishwa na klabu ya Azam.
#UFMUpdates
Nahodha wa Simba SC, John Bocco amefanikiwa kuwa mchezaji wa kwanza kupata ‘hattrick’ ya pili kwenye ligi kuu ya NBC baada ya kupachika nyavuni mabao matatu katika mchezo wao dhidi ya Tanzania Prisons.
Una maoni gani kuelekea mbio za mfungaji bora msimu huu?
#UFMUpdates
Klabu ya Simba imemuongezea mkataba wa miaka miwili mlinzi wa kati, Henock Inonga ambao utamuweka klabuni hapo hadi mwaka 2025 baada ya mkataba wake wa awali kumalizika mwishoni mwa msimu huu.
#UFMUpdates
#SimbaSC
#UsajiliSimba
#HenockInonga
Benki ya Dunia imeikopesha Tanzania dola za Marekani milioni 535 sawa na shilingi trilioni 1.24 kwa ajili ya kutekeleza miradi miwili ukiwemo mradi wa nishati ya umeme vijijini na mradi wa kukabiliana na mafuriko katika bonde la Mto Msimbazi jijini Dar es Salaam.
#UFMUpdates
Kiungo mshambuliaji wa Yanga SC, Feisal Salum kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa instagaram amethibitisha kuondoka kwenye klabu yake ya Yanga.
#UFMUpdates
#YangaSC
#FeisalSalum
#Usajili
HOROYA vs SIMBA: Kwa ubora aliouonesha Beno Kakolanya kwenye mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Al Hilal na uzoefu alionao Aishi Manula kwenye mechi za Kimataifa, unatamani kumuona nani akianza kwenye mechi yao ya leo dhidi ya Horoya AC ya nchini Guinea.
#UFMUpdates
Simba Queens wameibuka mabingwa wa kwanza wa mashindao ya Ngao ya Jamii kwa Wanawake 2023 kwa ushindi wa mikwaju ya penati 4-5 dhidi ya JKT Queens baada ya dakika zote za mchezo kumalizika kwa sare ya 1-1.
#UFMUpdates
Mshambuliaji wa Yanga SC, Fiston Mayele na Winga wa Simba SC, Saido Ntibazonkiza wamelingana idadi ya mabao baada ya raundi zote 30 za Ligi Kuu msimu huu kumalizika kila mmoja akiwa na mabao 17.
Unadhani nani anastahili kutwaa kiatu cha mfungaji bora?
#UFMUpdates
Klabu ya soka ya Simba imemtambulisha Mshambuliaji, Willy Essomba Onana (23) raia wa Cameroon kwa mkataba wa miaka miwili.
Onana amejiunga na Simba SC akitokea klabu ya Rayon Sports ya Rwanda.
#UFMUpdates
Bingwa wa michuano ya Olimpiki wa Ujerumani Malaika Mihambo, mwenye asili ya Tanzania ameendeleza ubabe katika mbio ndefu za wanawake kwa kunyakua medali ya pili ya dhahabu ya Ubingwa wa Dunia kwa kuruka umbali mrefu zaidi wa mita 7.12 huko Eugene, Oregon.
Kuelekea mchezo wa nne wa hatua ya makundi Kombe la Shirikisho Afrika
#CAFCC
, Afisa habari wa klabu ya Yanga SC,
@alikamwe
amesema kiungo mshambuliaji wa klabu hiyo Bernard Morrison ameanza mazoezi na kocha wa viungo ili kutengeneza utimamu wa mwili.
#UFMUpdates
#BernardMorrison
Mchezo wa ufunguzi wa michuano ya Ligi ya Soka Afrika
#AFL
kati ya Simba SC dhidi ya Al Ahly ya Misri umemalizika kwa sare ya 2-2.
Mchezo wa marudiano utakaopigwa Jumanne wiki ijayo huko Misri ndio utaamua nani aingie katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.
#UFMUpdates
Klabu ya Yanga SC imepangwa kucheza na ya Rivers United ya nchini Nigeria katika hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika
#CAFCC
kufuatia droo iliyochezeshwa muda mfupi uliopita.
#UFMUpdates
“Hatujaliona jua leo tangu kunakucha …,” Ramadhan Ngoda akielezea hali ya hewa mjini Algiers, Algeria ambako Yanga SC atakipiga na mwenyeji wake USM Alger kwenye mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika ...
#UFMUpdates
#CAFCCFINAL
#CAFCC
MSAFARA WA YANGA SC: Mashabiki wa Yanga SC wamefika Dodoma na hapa wanapata chakula kabla ya kuendelea na safari wakielekea Kigali, Rwanda.
Mechi itachezwa Jumamosi hii saa 10:00 Jioni
#LIVE
107.3UFM Updates na YouTube channel ya UFMRADIOTZ
#CAFCL
#YangaSCSafarini
#CAFCL
Klabu ya Soka ya Yanga imefanikiwa kutetea taji lake la ubingwa wa Kombe la Shirikisho la Azam Sports
#ASFC
baada ya kuondoka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Azam FC kwenye mchezo wao wa fainali uliopigwa leo katika dimba la CCM Mkwakwani jijini Tanga.
#UFMUpdates
#ASFC
#ASFCFinal
Kiungo Mshambuliaji wa Klabu ya Soka ya Simba, Saido Ntibazonkiza amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Mei wa Ligi Kuu ya NBC msimu huu wa 2022/23, huku Kocha Mkuu wa klabu hiyo, Roberto Oliveira akichagukliwa kuwa Kocha Bora wa mwezi huo.
#UFMUpdates
#TuzoZaMwezi
Mchekeshaji Khaby Lame, anayeongoza kwa kufuatiliwa zaidi kwenye mtandao wa TikTok duniani, amepewa uraia wa Italia katika hafla iliyofanyika katika mji wa Kaskazini wa Chivasso karibu na mji wa Turin alikokulia.
Shirikisho la Soka nchini
@Tanfootball
limetangaza kuwa teknolojia video ya mwamuzi msaidizi (VAR) itatumika kwenye michezo ya vijana chini ya umri wa miaka 20 (U20) hatua ya nusu fainali kesho Julai 15, 2022.
#UFMUpdates
#ULIVE
#SportsBando
PAPE OUSMANE SAKHO 🤯
🇸🇳 Amefanikiwa kushinda tuzo ya goli bora la mwaka alilofunga dhidi ya Asec Mimosas kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho.
#CAFAwards2022
Klabu ya Simba SC imeondolewa rasmi kwenye michuano ya African Football League kwa faida ya goli la ugenini iliyoipata Al Ahly ya Misri.
Mchezo uliomalizika muda mfupi uliopita kati ya miamba hiyo ya soka Afrika umemalizika kwa sare ya 1-1 na kufanya idadi ya jumla ya mabao 3-3.
Afisa habari wa Yanga SC, Ally Kamwe amesema mazungumzo yanaendelea kati ya uongozi wa klabu hiyo na kocha wake msaidizi, Cedric Kaze baada ya mkataba wake kumalizika mwishoni mwa msimu huo.
Kamwe ameyasema hayo wakati akizungumza na 107.3 UFM redio asubuhi ya leo.
#UFMUpdates
Klabu ya Mbeya City kutoka viunga vya Sokoine jijini Mbeya imeshushwa rasmi daraja na Mashujaa wa Ziwa Tanganyika kutoka Kigoma kwa ushindi wa jumla wa mabao 4-1.
Mashujaa FC itashiriki Ligi Kuu ya NBC msimu ujao wa 2023/2024 huku Mbeya City ikishiriki Championship.
#UFMUpdates
Klabu ya Simba imefanikiwa kupata sare ya mabao 2-2 dhidi ya CSKA Moscow ya nchini Urusi katika mchezo wao wa Kimataifa wa kirafiki uliopigwa leo huko Dubai.
Magoli yote ya Simba SC yamepachikwa nyavuni na Habib Kyombo katika dakika ya 49 na 77 ya mchezo.
#UFMUpdates
#SimbaSC
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro ameikaribisha klabu ya AL Ahly ya Misri kuja kuwekeza katika Sekta ya michezo nchini Tanzania kwa kufungua Academy ya michezo ili kukuza na kuendeleza vipaji vya wanamichezo.
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) imewatangazia watu wanaohudumiwa na mtambo wa kuzalisha maji wa Ruvu Chini uliopo Bagamoyo, kuwa mtambo huo utazimwa kwa saa 36 kuanzia kesho.
Soma zaidi ...
#UFMUpdates
#DAWASA
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally amemtangaza mgeni rasmi katika mchezo wa Derby ya Kariakoo utakao zikutanisha Simba dhidi ya Yanga Jumapili wiki hii kuwa ni Kibu Denis.
#UFMUpdates
#SimbaSC
#KariakooDerby
#SimbavsYanga
Miamba ya soka nchini kutoka viunga vya Kariakoo Simba na Yanga watakutana kwa mara ya kwanza Novemba 5 mwaka huu katika mchezo wao wa Ligi Kuu ya NBC 2023/2024.
Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Almas Kasongo amebainisha hayo leo wakati akitangaza ratiba ya ligi kuu.
#UFMUpdates
Simba SC imethibitisha kufikia makubaliano na klabu ya Quevilly Rouen Metropole (QRM) ya nchini Ufaransa kumnunua mchezaji wake, Pape Sakho.
Taarifa iliyotolewa na klabu hiyo imemtakia kila la kheri Sakho kwenye timu yake mpya.
#UFMUpdates
#SimbaSC
#UsajiliSimba
#PapeSakho
Rais wa Shirikisho la Soka barani Afrika
#CAF
, Patrice Motsepe amelitambulisha rasmi Kombe litakalokabidhiwa kwa bingwa wa michuano ya Ligi ya Soka barani Afrika
#AFL
.
Unadhani hili kombe litachukuliwa na nani?!
#UFMUpdates
#AFL
#CAF
#FIFA
Beki wa kati wa Uganda Cranes, Gift Fred (24) amejiunga na Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga SC.
Gift ambaye amekuwa nahodha katika klabu ya SC Villa inayoshiriki Ligi Kuu ya Uganda amesaini mkataba wa mwaka mmoja akiwa mchezaji huru.
#UFMUpdates
Yanga SC ya Tanzania imefuzu kucheza fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kuiondosha kibabe Marumo Gallants ya Afrika Kusini kwenye michuano hiyo.
Klabu ya soka ya Azam imeingia makubaliano ya ushirikiano na klabu ya soka la wanawake ya Baobab Queens ya Dodoma ikiwa ni utekelezaji wa agizo la kikanuni la leseni za vilabu kutoka Shirikisho la Soka barani Afrika CAF.
#UFMUpdates
#AzamFC
#BaobabQueens
Ukurasa rasmi wa Ligi Kuu ya Hispania La Liga, umeweka taarifa ya kuipongeza
@yangasc1935
kuwa mabingwa wa Ligi Kuu ya NBC kwa mara ya 28 kwenye historia ya klabu hiyo.
La Liga na Yanga waliingia makubaliano ya ushirikiano mnamo Mei 31 mwaka 2020.
MAPUMZIKO |
#CAFCC
Wananchi wanatakata katika dimba la Benjamin Mkapa katika dakika 45 za kipindi cha kwanza kwa kumfunga
#Kunguru
aliyeshindikana Dar es salaam.
Yanga 2-0 TP Mazembe.
Tupo
#LIVE
YouTube Channel ya UFMRADIOTZ na 107.3 UFM Radio.
#UFMUpdates
#CAFCC
#CCC
#CAF
Afisa habari wa Yanga SC, Ali Kamwe amesema mzigo wa jezi mpya za klabu hiyo zitakazotumika msimu ujao wa mwaka 2023/2024 tayari zimewasili bandarini jijini Dar es salaam.
Amesema hafla ya kufanya utambuilisho wa jezi hizo itafanyika mwanzoni mwa mwezi ujao.
#UFMUpdates
Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Lazaro Komba ametoa saa 6 kwa wakazi wa Kijiji cha Kasanga kurejesha zaidi ya gunia 600 za mahindi waliyoiba wakati wa ajali ya lori lililopinduka jana kwenye mlima wa kijiji hicho wakati likisafirisha mzigo huo kwenda bandari ya Kasanga.
#UFMUpdates
Christian Atsu, mwanasoka kutoka nchini Ghana aliyekufa baada ya tetemeko la ardhi kutokea nchini Uturuki, anazikwa leo nchini kwao Ghana.
Mazishi yake yanasimamiwa na serikali ya nchi yake na yatafanyika katika mji mkuu wa Ghana, Accra.
#UFMUpdates
“Chama hajaondoka na swala lake lipo kwa viongozi wa juu wakijaribu kulishughulikia lakini Chama hayupo kwenye safari hii ya kundi la pili la wachezaji wanaoelekea Uturuki …,” Ahmed Ally kwenye kipindi cha Sports Bando hapa 107.3 UFM Radio
#UFMUpdates
#SimbaSC
#SimbaUturuki
TOP SCORER: George Mpole wa Geita Gold, ameibuka kuwa Mfungaji Bora wa Ligi Kuu ya NBC baada ya kufunga bao moja kwenye mchezo wa mwisho dhidi ya Coastal Union na kumuacha aliyekuwa mshindani wake wa karibu Fiston Mayele wa Yanga aliyemaliza kwa magoli 16.
Klabu ya Soka ya Yanga imeshindwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika mbele ya USM Alger ya Algeria kufuatia faida ya goli la ugenini.
Katika mchezo wa kwanza ulimalizika kwa Yanga kufungwa 2-1 wakati mchezo wa pili wakishinda 1-0 na kufanya jumla ya magoli 2-2.
#CAFCC
Simba SC imeibuka bingwa wa Ngao ya Jamii 2023 kwa ushindi wa mikwaju ya penati 3-1 dhidi ya Yanga SC baada ya dakika 90 kumalizika bila kufungana.
Katika mikwaju ya penati iliyopigwa Golikipa wa Simba, Ally Salim amefanikiwa kuzuia penati tatu.
#UFMUpdates
#NgaoYaJamii2023
Baada ya miaka 25 Klabu ya Yanga SC imefanikiwa kutinga hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika
#CAFCL
kwa ushindi wa magoli ya jumla 3-0 dhidi ya Al Merrikh ya Sudan baada mchezo wa mkondo wa pili kumalizika leo kwa ushindi wa 1-0 katika dimba la Azam Complex.
#UFMUpdates
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika
#CAF
limemtaja Golikipa wa Yanga SC na Timu ya Taifa ya Mali, Djigui Diarra kuwa miongoni mwa magolikipa 10 wanaowania Tuzo ya Golikipa Bora Mwaka 2023 barani Afrika.
Watu wanne wamefariki dunia na wengine 21 wamejeruhiwa kwenye ajali iliyohusisha basi dogo la abiria aina ya Hiace kupinduka katika eneo la Kyetema, lililopo katikati ya Kata za Bujugo na Kemondo wilayani Bukoba.
Klabu ya soka ya Yanga itashuka dimbani leo dhidi ya USM Alger ya Algeria katika mchezo wake wa mkondo wa kwanza wa kuwania kutwaa ubingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika
#CAFCC
.
Tutakuwa
#LIVE
kwenye YouTube channel ya UFMRADIOTZ na 107.3 UFM kuanzia saa 9:00 alasiri.
#UFMUpdates
#BreakingNews
: Mgombea Ubunge wa CCM jimbo la Mpendae Zanzibar, Salim Turky (Mr. White) amefariki dunia muda mfupi uliopita usiku huu wa kuamkia Septemba 15, 2020.
Taarifa za chanzo cha kifo chake bado hazijafahamika, endelea kufuatilia kurasa zetu kwa habari zaidi.
#TANZIA
KILELE CHA SIMBA DAY 2020
Kinachoendelea muda huu kupitia
#AzaSports2
ni hafla ya chakula cha usiku inayojumuisha viongozi wa Simba, wachezaji wa timu ya wanaume na wanawake Simba Queens huku shughuli hiyo ikihudhuriwa na wageni Vital’O kutoka Burundi
#SimbaSC
#SimbaDay2020
Klabu ya Soka
@azamfc
imemtambulisha kiungo mshambuliaji James Akaminko, aliyesaini kandarasi ya miaka miwili akitokea Great Olympic ya Ghana.
Mghana huyo mwenye umri wa miaka 26, amewahi kucheza katika timu za US Tataouine (Tunisia), Ashanti Gold, Medeama na Tema Youth (Ghana)
Yanga SC imethibitisha kuachana na mchezaji wake Abdallah Shaibu (Ninja).
Katika taarifa iliyotolewa na klabu hiyo, imemshukuru Ninja kwa mchango wake katika kipindi chote alichokuwa akiitumikia Yanga SC.
#UFMUpdates
#UsajiliYanga
#YangaSC
#AbdallahShaibu
@yangasc
Simba SC imetangaza kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kati, Jean Baleke kutoka Jamhuri ya Kidemokasia ya Congo kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Nejmeh ya Lebanon alikokwenda kwa mkopo mwanzoni mwa msimu huu akitokea TP Mazembe ya DRC.
#UFMUpdates
#UsajiliSimba
#SimbaSC
YANGA VS IHEFU: “Ihefu tuna deni nao, hakuna mahali ambapo sisi tutafanya nao mzaha …” maneno ya afisa habari wa Yanga SC,
@alikamwe
kuelekea mchezo wao dhidi ya Ihefu SC utakaopigwa Jumatatu wiki ijayo.
Tazama video ...
#UFMUpdates
#YangaIhefu
Uongozi wa Singida Big Stars FC umefanya makubaliano ya kibiashara ya kuuza hisa zake kwa uongozi wa Fountain Gate Academy.
Makubaliano hayo yameambatana kubadilisha jina kutoka Singida Big Stars FC kuwa Singida Fountain Gate FC (The Big Stars).
#UFMUpdates
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Mzee Nyamka amesema mfumo wa kuajiri watumishi wa jeshi hilo kwa kigezo cha kupitia mafunzo ya jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ni mzuri kwa kuwa unawasaidia kupata vijana walio na uzalendo na utayari wa kutumikia Taifa.
#UFMUpdates
Klabu ya soka ya Simba imetangaza ratiba ya michezo yake miwili ya kirafiki ikiwa Dubai ambapo Jumapili wiki hii imepanga kucheza na CSKA Moscow inayoshiriki Ligi Kuu nchini Urusi na Ijumaa watakipiga dhidi ya Al Dhafra ya Dubai.
Mechi zote ni saa 10:00 jioni.
#UFMUpdates
Jeshi la Yanga SC litakaloanza kwenye kwenye mchezo wa fainali Kombe la Shirikisho Afrika
#CAFCC
.
Diara Djigui
Djuma Shabani
Joyce Lomalisa
Bakari Mwamnyeto
Ibrahim Bacca
Dickson Job
Tuisila Kisinda
Salum Abubakar (Sure Boy)
Fiston Mayele
Mudathir Yahya
Kennedy Musonda
Katika mbio za kukisaka kiatu cha dhahabu cha mfungaji bora wa Ligi Kuu ya NBC msimu huu Mshambuliaji wa Yanga SC, Fiston Mayele amefunga goli lake la 17 katika mchezo wao wa mwisho dhidi ya Tanzania Prisons unaoendelea muda huu.
#UFMUpdates
#BreakingNews
: William Ruto wa Chama cha UDA ametangazwa kuwa rais mteule wa Kenya baada ya kushinda uchaguzi mkuu kwa asilimia 50.49 akimuacha mpinzani wake wa karibu Raila Odinga wa Muungano wa Azimio aliyepata asilimia 48.85 ya kura zote.
#KenyaDecides
#KenyaDecides2022
“Ukiangalia tulianza na mabeki, tukaja viungo na tumetambulisha winga kwa hiyo maana yake haturudi nyuma tena …,”
@alikamwe
kwenye kipindi cha
#ULIVE
hapa 107.3 UFM Radio.
Unadhani atakayetumia jezi yenye namba sita msimu ujao atacheza nafasi gani?
#UFMUpdates
#UsajiliYanga