Kila SILAHA itakayofanyika juu yako HAITAFANIKIWA, na kila ULIMI utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa MKOSA. Huu ndio URITHI wa watumishi wa Mungu, na haki yao!💪🏽(Isa 54:17 )
Namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa UPENDO wake kwangu. Nakushukuru KIPEKEE Mhe Rais SAMIA kwa IMANI hii kubwa kwangu. Ahsanteni sana wadau kwa kunipokea. Nina kuahidi Mhe Rais SITAKUANGUSHA! Najua na kuheshimu mategemeo yenu kwangu, Mungu atanisaidia KUYATIMIZA. SITAWAANGUSHA!
Aaaah kiroboto🤣🤣ulishindwa akiwepo godfather utaweza leo?!!? Kina wenyewe shekh! Lakini ni kawaida punda roho ikiwa inaacha mwili hutupa mateke 🎼NONSENSE!!
Maisha mazuri ukiwa na furaha, lakini maisha ni mazuri zaidi na yana maana zaidi kama kuishi kwako kuna wafanya watu wengine pia wafurahi! Nawatakia Pasaka njema!
Sio rahisi kupata maneno sahihi ya kusema kwa sasa. Itoshe kusema hili ni pigo kubwa kwa wanaMtama na kusini kwa ujumla! Mwamba umeanguka! Pumzika kaka yangu!😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭
What a loss!!!🙆🏿♂️🙆🏿♂️😭😭! Nakumbuka sana Upendo, Malezi na Busara zako nikiwa Mkuu wa Wilaya Masasi!Aaah, mwamba mwenye sifa halisi za kusini, what a loss!! Pumzika baba!
Kama ambavyo kifo ni hakika kwa kila kiumbe ndivyo ambavyo mwisho wa kila jambo ni hakika pia! Mwisho wa wema ni fahari na mwisho wa ubaya ni aibu! Mungu hadhihakiwi!
Leo nimefanikiwa kumsindikiza kupumzika mtu aliyeokoa nisifukuzwe shule kwa kukosa ada na aliyeokoa nisifukuzwe/ nisiondoke CCM! Pumzika Mzee Mkapa, Msalimie Mzee Nnauye, mwambie umemaliza kazi aliyokuachia kwangu! Ahsante sana!
Kwenye siasa ukiona unapiga kelele hujibiwi fikiri mara mbili! Ni sawa na draft ukiona unaruhusiwa kula tu, kinachofuata inaweza kuwa majanga🤣🤣🤣🤣🏃🏾♂️🏃🏾♂️🏃🏾♂️🤦🏾♂️
🎼🎶🎶🎹🎼Nikumbushe wema wako nisijelaumu, nikumbushe ukuu wako wakati wa magumu, nikumbushe shuhuda zako ili nikusifu...niimbe wimbo wa sifa katikati ya machozi...🎼🎹🎼🎶🎶
Mdogo wangu Paul, Karibu sana kwenye Uongozi wa juu kabisa wa Chama chetu. Nina hakika umetumia vizuri muda wa likizo, and now you are ready for the job! HONGERA kwa kuaminiwa na nakutakia kila lakheri!
Uteuzi wa Mhe. Hussein Bashe na Mhe. Simbachawene ni katika teuzi bora kabisa. Ninawapongeza na kuwatakia majukumu mema! Kaka January karibu back bench, Hongera kwa utumishi wako!
Kila PITO lina SABABU yake! Shida kubwa ni kujua SABABU/KUSUDI la Mungu kuruhusu mapito flani maishani. Mungu nifundishe kuyajua MAKUSUDI ya kila PITO ili moyo wangu ukutukuze katika kila PITO!
Mwanangu kumbuka …Madaraka hayabadili watu ila huonyesha uhalisia wa mtu🤦🏾♂️. Chunguza sana marafiki wanaokuzunguka wanaweza kuwa marafiki wa madaraka uliyonayo na sio marafiki zako wewe!
Vyovyote iwavyo siasa lazima iendelee kuwa ni shughuli ya kushindanisha akili katika kutatua changamoto zinazoikabili jamii husika! Mkiacha kutumia akili, siasa inageuka kuwa sumu itakayoangamiza jamii husika! Lazima tuseme HAPANA!
Utotoni ukiona mtu anatishia sana kwa maneno tulikuwa tukimpuuza maana mfanyaji HUSEMA mara moja na KUTENDA, maneno mengi ya ICC, kila siku ni vitisho vya kitoto. Kura na maamuzi yanafanywa na Watanzania sio Mahakama ya Kimataifa ya Kesi za Jinai!
Usivunje mtungi kuua panya aliyemo ndani ya mtungi, busara ni kuinamisha mtungi taratiiiiiiiiiiiiiiiiibu panya atatoka mwenyewe! Kukata kichwa cha kobe kunahitaji timing!!
Kumekuwa na MJADALA mkubwa kuhusu USHAURI wangu juu ya Wabunge wa Viti Maalum waliotokana na Chadema:- kwa kifupi SWALA HILI NI LA KISHERIA {Katiba ya Chadema na Katiba ya Nchi}, Sheria hizo NDIZO ZINAZOAMUA/TAFSIRI HATMA YAO. .....
Kila jambo kuna majira, na wakati kwa kila kusudi. Wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa. Kupanda na kung’oa. Kubomoa na kujenga. Kulia na kucheka. Kunyamaza na Kunena. Kupenda na kuchukia. Wakati wa vita, na wakati wa amani. Tumia wakati wako vizuri, kwani hakuna lidumulo!
Umeacha alama kubwa! Nimejifunza mengi kwako, Rafiki, Mshikaji, Kiongozi na Mzazi! Ulinifundisha kuwa KUKATA TAMAA NI DHAMBI! {Msalimie Mzee Sitta, mkumbushe kile kikao chetu Cha mwisho nyumbani kwako}Pumzika kwa Amani Dr. R.A Mengi.
Unahitaji taasisi imara na thabiti kama CCM kutengeneza mtu wa aina yako. Sina mashaka October 2020 , ushindi mapemaaaaaaaa! Zanzibar na Muungano viko salama kwako! Kila lakheri Dr Hussein Ally Hassan Mwinyi!
Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya ajali ya gari iliyosababisha vifo vya Maafisa Habari, Waandishi wa Habari wa Mwanza na Wananchi. Natoa pole kwa Familia za Marehemu, Waandishi wa Habari wote, ndugu, jamaa na marafiki. Mungu aziweke mahali pema roho za marehemu wote, Amina.
Siku ya mwisho uliniambia “ Napalepe maanaake hata usiku uwe mrefu vipi kutakucha!” Kila nikikumbuka maneno haya ninapata nguvu ya kusonga mbele! Ni miaka 17 sasa na maisha hayajawa Sawa tena toka uondoke! Pumzika kwa Amani, baba, Rafiki,Mzalendo na mmakonde wa kweli!
Mwenyezi Mungu kaniokoa na ajali mbaya leo asub, wakati natoka Mtama kuelekea kwenye kikao cha Chama Liwale. Namshukuru sana M/Mungu. Nawashukuru sana wananchi wa kijiji cha Kibutuka, wamenisaidia sana, Upendo wenu umenigusa sana! Familia,Viongozi na marafiki nawashukuru sana!