Nishati
@Nishati2017
Followers
55K
Following
59
Media
2K
Statuses
5K
Official Page-Ministry of Energy in Tanzania.This page will be useful in providing correct and latest information on Energy Sector. Visit http://www.nishati.go
Tanzania
Joined May 2013
Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Salome Makamba amezindua mradi wa Nishati Safi ya Kupikia katika Shule ya Sekondari Bunge Wasichana iliyopo jijini Dodoma leo tarehe 04.02.2026. Mradi huu umetekelezwa chini ya Wizara ya Nishati na umegharimu takribani shilingi Milioni 30.
1
0
1
Hayo yameelezwa na Mhandisi Felista Ndabita kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), wakati wa ziara ya kikazi iliyofanywa na Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) kwa lengo la kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa mradi huo.
1
0
1
Maandalizi uchimbaji visima vya gesi asilia Mtwara yafikia zaidi ya asilimia 90 Maandalizi ya uchimbaji wa visima vitatu vya gesi asilia katika Kitalu cha Mnazi Bay kilichopo mkoani Mtwara yanaendelea vizuri ambapo hadi kufikia Februari 03, 2026 yamefikia zaidi ya asilimia 90
1
0
1
Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Salome Makamba akiwasili katika viwanja vya shule ya Sekondari Bunge Wasichana jijini Dodoma na kupokelewa na viongozi mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa mradi wa nishati safi ya kupikia katika shule hiyo leo tarehe 04.02.2026
0
0
2
sambamba na kubainisha fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo katika nchi washirika pamoja na namna bora ya kuzifikia. Maadhimisho hayo yamefunguliwa rasmi na Waziri Mkuu wa India, Mhe. Narendra Modi, katika Jimbo la Goa nchini India,
0
0
1
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, leo Januari 27, 2026 ameshiriki katika ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Nishati India (India Energy Week – IEW 2026), yanayolenga kujadili na kuweka mikakati ya pamoja ya kukuza sekta ya nishati kwa njia endelevu na shirikishi,
2
0
1
Aidha, amesema kuwa hadi kufikia Desemba 2025, zoezi la uthamini wa fidia kwa wananchi hao limekamilika na kwa sasa lipo tayari kwa hatua ya uhakiki na uwekaji wazi wa jedwali la wafidiwa.
0
0
0
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema kiasi cha Sh. Bilioni 6,02 kinatarajiwa kuwalipwa na serikali kwa wananchi 347 wa Vijiji vya Lifua, Liugai na Masimavalafu wilayani Ludewa, Mkoa wa Njombe, waliopisha utekelezaji wa mradi wa umeme, katika mwaka wa fedha 2026/27
1
0
1
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi akiwasili katika ukumbi wa Bunge tayari kwa ajili ya kushiriki kikao cha kwanza cha mkutano wa pili wa Bunge la 13 kinachoanza leo Januari 27, 2026 bungeni jijini Dodoma.
0
0
1
Kikao hicho kimefanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati, Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, na kuhudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesm Mramba, Mwenyekiti wa Bodi ya PBPA, Dkt. Lutengano Mwakahesya, Mtendaji Mkuu wa PBPA, Bw. Erasto Simon.
0
0
0
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, leo Januari 26, 2026 amefanya kikao kazi na Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) chenye lengo la kujadili mikakati ya kuimarisha na kuendeleza utendaji wa wakala huo.
1
0
0
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi leo Januari 23, 2026 ameongoza kikao kazi cha Wataalam wa Wizara kuzungumzia mikakati ya kuendeleza Sekta ya Nishati kwa mwaka 2026. Kikao hicho kimefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Nishati, Posta Jijini Dar es Salaam.
0
0
0
Akizungumza leo Januari 22,2026 jijini Dodoma wakati akifungua Baraza Kuu la 55 la Wafanyakazi wa TANESCO,Waziri Ndejembi amesema maboresho yanayofanywa na Shirika yametoa matumaini mapya kwa wananchi na kuimarisha utendaji.
0
0
0
WAZIRI wa Nishati,Mhe.Deogratious Ndejembi,amelipongeza Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO)kwa hatua kubwa za kuboresha huduma kwa wateja,akisema mageuzi yanayoendelea ndani ya Shirika hilo yanadhihirisha dhamira ya dhati ya kuimarisha upatikanaji wa umeme na kuongeza ufanisi
1
0
0
Mkutano huo umeandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na umewahusisha Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri pamoja na Maafisa Lishe kutoka mikoa yote nchini.
0
0
0
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, leo tarehe 22 Januari, 2026, amezungumza katika Mkutano wa Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 unaofanyika katika Ukumbi wa Mabeyo, jijini Dodoma.
1
0
0
Taarifa za Wizara ya Nishati kuhusu muundo na majukumu ya taasisi hizo kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini. Kikao hicho kimefanyika leo Januari 21, 2026 katika kumbi za Bunge jijini Dodoma chini ya Mwenyekiti wa kamati, Mhe. Subira Mgalu.
0
0
0