Very good is not enough when we have excellent .Hatuta nyamaza wala kupoa mpaka pale Azimio la Bunge la Mkataba huu wa kijambazi litakapofutwa na Bunge na zaidi serikali ya CCM kusitisha utekelezaji wa IGA haramu.
Hatutafuti Mshindi tunalinda Raslimali zetu.
Aluta Continua..
Msifadhaike wala Msikate tamaa. Nakuhakikishieni kwamba Karibu kuna Pambazuka maana Mungu wetu hasemi uwongo. Karibu tunafika....USALAMA WA RASILIMALI ZA WATANGANYIKA NI KIPAUMBELE CHETU.
Ni kweli nimepata complaint ninayotakiwa kujibu ndani ya siku 21. Tuhuma zangu katika complaint hiyo zinahusiana na mkataba wa bandari ambao binafsi nimekuwa nikiupinga kutokana na mapungufu yake. Nitazingumza na vyombo vya habari kuweka msimamo wangu juu ya hili.
Aluta Continua
Biblia Takatifu imeandika mara 365....USIOGOPE....uwoga ni dhambi....tutapitishwa tena na tena kwenye bonde la uvuli wa Mauti kabla ya kuufikia ukombozi kamili. Mungu yupo nasi.
Aluta Continua...freedom Ascerta
Tanganyika is coming tommorrow
Bak Mwabukusi
Shambani
Busokelo.
Asanteni sana wenzangu wote tulioshirikiana katika shauri hili mpaka kufikia hitimisho na kusubiri hukumu. Asante sana senior Mpale Mpoki, Philip Mwakilima na Livino Ngalimitumba. Tukutane tena tarehe 7th August 2023 kwa ajili ya hukumu.
Kuna Watu wamevamia ofisi yangu Usiku wa Jana tarehe 24/5/24 .Wamevunja na kuchukua vifaa vyangu vya kazi...Desk Tops,Printers, TV yani unaiba hadi efd Machine kweli?
Nimeripoti Police wamenipa Ushirikiano yeyote mwenye taarifa ni Juze kupitia No.0765 742595
Nguvu kubwa zinazotumika kumshambulia huyu mwamuzi zingetumika kudai Katiba Mpya Nchi ingeshakuwa na Katiba Mpya.
Tuliokuwa tukitizama mechi kwenye vibanda umiza na TV za Chogo wote tunaona mwamuzi kakosea.Hata wezi wa kura wanamlaumu. DAI KATIBA MPYA NA TUME HURU YA UCHAGUZI.
Hii ndiyo Mbeya ndugu achaneni na yule bingwa wa kushindwa na Dhaifu na hafifu..
Huu ndiyo ukweli Mbeya iliitwa ikaitika acheni wajifariji kwa kupotosha mitandaoni ila mwambieni akatafute kazi nyingine ya kufanya ...HUWA HATUDANGANYI.....KATIBA MPYA NDIYO MSINGI WA YOTE.
Upuuzeni Upumbavu huu. Huyu aliyeandika ujinga huu anajaribu kuvuruga Kongamano la kuokoa bandari zetu na agenda ya katiba mpya Mwanza hapo kesho. Nawajulisha kwamba nawaheshimu CHADEMA na siwezi kuongea kipumbavu namna hii. Wametengeneza wenyewe wanasambaza wenyewe.
KESHO NI SIKU MUHIMU KWA WATANGANYIKA KUHUSU MSTAKABALI WA MALI ZAO.
FIKA MAHAKAMA KUU MBEYA KUONESHA MSHIKAMANO.
NI WAJIBU WA SERIKALI YA TANZANIA KUTAMBUA KWAMBA, KUWA WASIMAMIZI WA MALI ZA TANGANYIKA HAKUWAGEUZI KUWA WAMILIKI WA MALI HIZO.
Aluta Continua...
Ndiyo Naemda kuandamana sasa ..Mimi Naanzia Uyole .Katiba Mpya,Tume Huru,Sheria Mbovu za uchaguzi,Mkataba Mbovu wa Iga ya Tanzania na Dubai,Haki ya Wazawa kumiliki Ardhi na Wamasai kuishi Ngorongoro.NAONA WAMEANZA KUTOA MLIO...HIZI RASHASHA WASUBIRI MASIKA..ALUTA CONTINUA
A typical Nyakyusa Mother. Hakupenda uzembe,uwoga,ujinga au dhuluma...alichukia Uvivu na kuhimiza Ibada...Ukiwa kwake upende usipende utake usitake saa Moja Jioni ni Muda wa Ibada.
Endelea kupunzika kwa Amani Mama yangu Tabitha Ikunda Pigale.
@ExMayorUbungo
Nitajitolea bure huduma ya kisheria kwenu nyote ...na hatuta ishia hapo kwa kitendo hiki anastahili kuburuzwa Mahakamani kwajina Lake ni uhalifu huwezi kushambulia whistle blowers kwa issue zinazo athiri usalama wa raia.
Usalama na ulinzi wa uhai ni jukumu la kila mmoja
Maoni haya ya Mahakama hayahusiani na uamuzi wa kesi wala hayawezi kuathiri hadhi au matokeo ya kesi. Kwani Kesi huamriwa kwa uzito wa hoja na Ushahidi uliowasilishwa na kupokelewa Mahakamani kwa mujibu wa sheria.
Kupitia Maandamano haya nimezidi kujifunza ....Wale wote munaobeza na kudhihaki ninawaambia hakuna Jiwe litakalo sazwa.Najua kuna watu wanapumua Chuki.Sisi tuko pale pale.IGA ni haramu Katiba Mpya,Haki ya Kumiliki ardhi,tume Huru,Wagombea huru.Hatutababaika wala kutetereka
Sintakuwa na Sababu yeyote halali ya kutounga mkono Msimamo madhubuti wakutumia nguvu ya Umma kudai mabadiliko ya Katiba.Lazima tusimame kwa pamoja Kulia na wanao lia....na Kutabgaza Mwaka wa Ukombozi .Hili tamko inahitaji uwendawazimu kutolielewa.
Naam Punde Tunaingia Mahakama ya Rufani ya Tanzania kuendelea na soft issues za Mkataba wa Bandari wakati huo Hard Issues ambazo ni mikutano na Maandamano yasiyo na ukomo inaendelea.
SAY NO TO THE EXPLOITATIVE IGA.
BAK Mwabukusi
Shambani Busokelo
Tukutane Buhongwa Jiji la Mwanza Muda huu...Dai Katiba Mpya...Tume Huru...Kufutwa kwa IGA ya Tanzania na Dubai na Kuheshimiwa kwa Haki ya Watanganyika Kumiliki Ardhi na kufaidi Raslimali asili zilizo ndani ya Mipaka yao.MAPAMBANO YANAENDELEA
Mkutano nyumbani Kandete Mbeya leo, Agenda ni kupinga mkataba wa IGA na madai ya katiba Mpya. Sasa tujiandae kwa tamko ya siku ya maandamano kesho kwenye press na waandishi wa habari.
Nimemfuata huyu mkora aliyejiteka mara kadhaa,kujipiga,kujijeruhi na wakati mwingije kujitupa vichakani...ANIAMBIE SIRI YA KUJITEKA...anasema kwamba Mh.Waziri amuite ili amuoneshe baadhi ya waliomteka kwa misimamo yake ya Kisiasa na aache majibu mepesi kwenye Maswali magumu.
Ndugu zangu JWTZ naomba tarehe 23 na 24 mukitoka Kambini musirudi mpaka tutakapo pata Katiba.Ninyi nanyi ni wahanga wa Vikokotoo,Katiba Mbovu na Ubadhirifu.Hii nijia Mungu anawapa kwamba Muungane na Baba zenu ,Kaka Zenu kuondosha hizi familia tano kwa Maandamano ya amani.
Hata ikilazima Ardhi na Mbingu kugusana mimi nasimama na Wamaasai.Ngongoro ni nyumbani kwao.( Even if it means the sky to fall ..I stand with Maasai...Ngongoro is their home it belongs to them) stop the unlawfull eviction and victimization of the Maasai Community in Ngorongoro
Niko na Mdude Mpaluka, Abdul tuko Arusha...Tumewasili Arusha IGA NI HARAMU,KATIBA NI MSINGI WA HAKI NA WAJIBU ZOTE,MABADILIKO YA SHERIA YANAKIUKA KATIBA ,NGORONGORO IS FOR MAASAI.ARUSHA INAUNGURUMA. NITAKUWEPO...NITAANDAMANA NGARENARO YOOOTE MKUJE TUANDAMANE KWA MASLAHI YA TAIFA.
Nitakuwepo Mwanza:
1.Kuonesha Mshikamano
2.Kuwaambia Viongozi kwamba demokrasia na Ulinzi wa Raslimali unakamilishwa na Katiba Bora
3.Mkataba wa TZ na Dubai kuhusu uendeshaji wa Bandari ni haramu.
4.Marekebisho ya sheria za Uchaguzi yaanze na Uandikaji wa Katiba.
Nipo na
@mdudechadematz
na
@LusakoAlphonce
Tunatafakari Madhila ya wakosoaji wa Bandari.Tunakuja na tamko la kina kuhusu ulaghai na uwekezaji wa Bandari ya Dar es Salaam.Hatuta nyamaza mpaka tutakapo inusuru Bandari yetu.Hatuta ruhusu wazalendo kutiwa hofu.SAY TANGANYIKA
ASANTE KWA KUPAZA SAUTI.
Licha ya Ugumu ,Mateso na fadhaa tunazopitia tutaendelea kutabasamu huku tukipambana bila kuchoka.
Hatuta nyamaza wala kuruhusu dhuluma kutamalaki.
Tutapambana mpaka tone la mwisho
Kesho nitaongea na vyombo vya habari kuhusu kinachofuata.Aluta Continua.
Mch.Mbarikiwa Mwakipesile Leo ameungana na Familia yake baada ya kukamilisha malipo ya faini kwa kifungo tunachoamini ni kinyume cha sheria.Mchakato wa rufaa unaendelea.
Tunaposimama kukataa dhuluma tunatimiza wajibu wetu kwani hatuna nchi nyingine isipokuwa hii. Hatutakiwi kutafuta umaarufu wa mtu binafsi bali kunatafuta Haki. Tulinde Raslimali zetu kwa kuhakikisha uwekezaji unakuwa wa maslahi kwa kuwa hatuna rasilimali zingine isipokuwa hizi.
Leo Asubuhi Nimetembelewa na Nguli wa Siasa za Upinzani na Kamanda wa CHADEMA katika Mkoa wa Mbeya ndugu John Mwambigija. Alifika kunisalimu na kunitiq Moyo.Tumeongea,Tumefurahi na Mwisho tuka agana.
Leo niko na
@mdudechadematz
na
@JumaAbdukarim
Arusha nawaonesha kwanini Ngarenaro ni kubwa kuliko Arusha.
Katiba Mpya...IGA ni haramu ..Ngorongoro if for Maasai...Mali ya Urithi haiuzwi.
Maandamano ni lugha adhimu wanayo ielewa watawala wa kiafrika.
Ni mwendawazimu tu atakaye shindwa kuuelewa ukweli huu...kama hutaki kuandamana baki na mkeo chumbani waache CHADEMA watumie haki yao ya kikatiba...Katiba Mpya...Miswada Mibovu iondolewe Bungeni...IGA ni Haramu. NITASHIRIKI NA KUJUMUIKA.
Kuwazuia
@ExMayorUbungo
na
@MalisaGJ_
ni matumizi mabaya ya dhamana na Madaraka. Hakuna kosa lolote wala uzushi walio ufanya na yote waliyosema yako bayana .Ni jukumu la kila Mtanzania kupigia kelele dhuluma hii. Is 4R timidity?
Nimepokea Rasmi Wito wa Kufika Mbele ya Advocate Committee mnamo tarehe 20 na 21 kwa ajili ya Usikilizwaji wa Shauri hili kufuatia Malalamiko ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi yangu na Maombi yake ya Jina langu kuondolewa katika Orodha ya Mawakili.
Aluta Continua...
Tunayaweza Mambo yote katika yeye atutiaye Nguvu.Mungu akiwa upande wetu ni Nani Atasimama dhidi yetu?
Jipe Moyo Mkuu Mateso na dhihaka zao hazitakuwepo tena.
Tumeupokea na kuuheshimu uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania .Wateja wetu wametuelekeza kukata rufaa Mahakama ya Rufani mara moja. Na sisi mawakili tumeshalifanyia kazi.
Je hatuko salama? Je tuko salama? Taarifa hii ni ya kusikitisha.? JE tuna haki ya kuhoji? Tumhoji nani? Je tumejifunza lolote kuhusiana na hili tukio? Naam cha muhimu siyo kufa ni je tunakufaje...? RIEP Ole Mushi .Tuonane Ng'ambo ya Mto. ALUTA CONTINUA
Maamuzi ya Rufaa ya Mteja wetu yametoka Leo. Na kwamba
1.Atalipa faini.
2.Tukate rufaa Mahakama ya Rufani Tanzania dhidi ya faini na adhabu.
3 Alifuata taratibu za Usajili wa dhehebu na alinyimwa fursa ya Rufani kwa Waziri
4.Anaonewa na ni Muhanga wa siasa za Mbeya.
Ndugu Mkuu wa Mkoa na OCD Mbeya kwa lolote baya litakalo tupata mutawajibika binafsi kwa Kauli zinazohamasisha maauji ya kimbari. Mmehamasisha kushambuliwa kwa watu wenye maoni tofauti kisiasa...kumbukeni Mbeya kwenu ni kazini kwetu Mbeya ni Nyumbani. Mungu ni Mwema.
Hivi Rais Mtanganyika anaweza kwenda kugawa ardhi au Mali ya Asili ya Wazanzibar kwa wageni? Na wazanzibar na wanasiasa wake wakamshangilia? Najiuliza na wewe jiulize kuhusu wanasiasa wetu wa Tanganyika na uwajibikaji wao ili mwisho tusioneane.
Tunahitaji Maelezo haya Magari ya Umma yalikuwa yanafanya nini katika msafara huu wa shughuli za kichama? Yanatoka idara gani? Na yako katika msafara huu kwa utaratibu gani na Gharama za lundo hili la msafara zinagharimiwa na nani?
NINAWAZA.
1.Bunge la JMT halina mamlaka ya kukabidhi raslimali za Tanganyika kwenye mikono ya DPW au mgeni yeyote.
2.Mamlaka ya Bunge la JMT ni ya kikatiba na kisheria.
3.Hakuna mwenye mamlaka kukabidhi raslimali asili za watanganyika kwa wageni.
4.Katiba Mpya haiepukiki.
Nimepokea Wito kutoka katika Kamati ya Nidhamu ya Mawakili ( The Advocate Committee) wa kufika Mbele ya Kamati kwa ajili ya Uamuzi mnamo tarehe 17/05/2024. Nitafika ili kupokea Uamuzi.
Kwa sakata la Babati Chanzo ni Katiba Mbovu iliyo tupa Bunge legalege.Nchi yenye Bunge legelege ni sawa na Lindo lenye mlinzi Kipofu.
Tunakwenda kwa kudra za Mwenyezi Mungu.Tunahitaji kupata KATIBA MPYA..TUME HURU ..ILI KUWA NA UWAJIBIKAJI KATIKA UTUMISHI WA UMMA.
Hata kama tuna Agenda Mia nane zinazotutofautisha lakini tukawa na nusu agenda inayo tuunganisha kwa maslahi ya Taifa letu tuungane katika Nusu hiyo tukishamaliza ndipo tukae chini kumaliza tofauti zetu .Adui yetu ni genge lililojificha CCM.
Hata Biblia takatifu inatuambia pale sadaka yako itakapokuwa ndipo Moyo wako utakapokuwa.Namimi nasema Pale kura yangu itakapokuwa ndipo nitakapohitajika kuwepo hadi hesabu zikamilike.KATAA MABADILIKO HARAMU YA SHERIA ZA UCHAGUZI.Dai katiba Mpya. HERI YA PASAKA WATU WA MUNGU.
Sisi tutawasilisha ili Yesu atende... UKWELI NI UKWELI tu haijalishi unakubaliwa au kupingwa na wangapi...UKWELI uko sahihi unajipigania na kujilipizia kisasi ukipuuzwa.
Kama reasoning hii ndiyo ya Waziri Mwenye Dhamana....basi tambua kwamba kama Taifa.....Tumepigwa anaongelea kiyoyozi kwa Madaha wakati hatujui hata kesho yetu Itakuwaje..ila yeye eti katoboa
Namshukuru Mungu nimefika salama mchana huu hapa Dar es salaam tayari kwa mkutano wa hadhara pale Temeke. Mliopo mbali muendelee kusogea ili kwa pamoja tujadili ubovu wa mkataba wa bandari zetu. Ni haki yetu kukusanyika na kujadili jambo la kitaifa kwa maslahi ya taifa.
Tuliwaambia Wamasai Nyumbani kwako ni Loliondo na Ngorongoro.Mumewafukuza mukitaka waishi kisela wakivaa mlegezo. Sasa haya Mambo ya kuwapangia hapana waacheni hamtaki warudisheni kwao.Vinginevyo waache waende maake naninyi mumeenda kwao na kutwaa ardhi yao😆
Sifungamani na Chama chochote cha siasa sizuiwi kusema ukweli watanganyika wenzangu , Njia ya kweli ya kutupeleka kwenye Ukombozi wa Kweli wa Taifa hili ni Katiba Mpya,Tume Huru na Haki ya wazawa kumiliki Raslimali . CHADEMA wanaamini katika Agenda hizi niwapinge kwa lipi?
Hitaji la Wananchi ni Katiba Mpya,Tume Huru ya uchaguzi na Kufutwa kwa mkataba haramu wa Serikali ya Tanzania na Dubai unaopora Raslimali Asili za Watanganyika .Tunahitaji kuheshimiwa kwa Haki ya wazawa kuishi na kuyatumia maeneo yao ya Asili.Hayo mengine yasubiri kwanza.
AMEPATIKANA. Tuna laani upumbavu huu wa kuteka na kudhuru watu kwa Maoni wanayotoa .Tutatoa tamko rasmi kwa watanzania kuhusu ukora huu na wahusika kesho sasa tutakabilianq nao kibabe na kwa namna wanavyotaka.Pole sana Mwamlima.
Baada ya mkutano wa jana pale Temeke sasa ni safari kurudi Mbeya kwa ajili ya kesi yetu ya bandari itakayoanza kusikilizwa kesho tarehe 25th Julai 2023. Wananchi wote mnaopinga mkataba mbovu wa bandari tukutane kesho saa tatu asubuhi mahakama kuu kanda ya Mbeya.
Asanteni🙏
SAUTI YA WATANZANIA.Dr Wilbroad Slaa,Askofu Mwanamapinduzi,Adv.Boniface Mwabukusi na Comrade Mdude Mpaluka Nyagali tuko arusha.Ngorongoro is 4 Maasai,KATIBA MPYA,IGA ni HARIMU ,Marekebisho ya sheria na ulaghai wa kisiasa.
CHADEMA WAMEANZA TWENDENI TUKAWAUNGE MKONO.
13.02.2024 - Mwanza
20.02.2024 - Mbeya
27.02.2024 - Arusha.
Serikali:
1. Ilete Mpango wa kupunguza gharama za Maisha
2. Kupeleka Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba .
3.IGA ya Tanzania na Dubai ni Haaramu.
Asanteni kwa Heri zenu Nyingi.Mungu awabariki.Tutege Masikio yetu Dodoma kuwasikiliza wakati Mijadala ya KWAKUWA inaendelea.
Wakimwaga Ugali basi wajue tutamwaga mboga.
Wakituletea Cheni ya Bandia Tutawalipa Noti za Bandia.KATIBA MPYA,TUME HURU HAKI YA WAZAWA KUMILOKI ARDHI.
TANGANYIKA MY MOTHERS LAND
Leo nimekutana na Wakili Msomi Senior Francis Stola Rais Mstaafu wa Tanganyika Law Society.
Tupo Mahakamani kuwasilisha wananchi maslahi ya Taifa.
bak mwabukusi
Shambani Busokelo.
BANDARI NI URITHI WETU.
Urithi Huenziwa Hauchezewi wala Kupewa Wageni.Tumerithi Tuwarithishe.
Rufaa ya Ndugu MADELEKA ni Jumatatu Tarehe 28/8/2023 Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala ya Arusha Mbele ya Mh.Jaji Masara kwa Usikilizwaji.
Hakuna sheria yeyote hapa Tanzania inayokataza hizi namba za 3D .Polisi ni wasimamizi wa sheria na siyo vinginevyo.Askari kama huyu unaruhusiwa kumshtaki kwa jina Lake binafsi na kumlazimisha kulipa fidia.
She is always there kwenye Mambo ya Msingi ya Taifa letu....halafu unamkuta kijana yuko busy kubet au kumfukuza Mangungu au Muwekezaji Simba...tufanye mambo ya msingi kwanza.
POLISI KUPITIA RCO Mbeya ACHENI KUTESA RAIA NA KUTEKELEZA MAJUKUMU KINYUME CHA SHERIA NA KATIBA.
Kitendo cha Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya kupitia RCO ambaye amebobea kwenye ukiukaji wa sheria na kutumia vibaya Cheo chake kinyume cha sheria na kukandamiza Raia wema na
Wanaume waerevu wakikristo wanafahamu kuwa Bila Yesu hauwezi Jambo lolote ....hii ndiyo inayoitwa prove them wrong.Taifa letu likiacha ushirikina ,ubabaishaji,upigaji na Mzengwe katika Soka tunavijana wanaviwango bora sana....tusinge hangaika kuokoteza wachezaji wa Stars.
Sihitaji kushukuru kwa yeyote kwa kuitumua haki yangu ya kikatiba .
Nikichekesho kumshukuru aliyeshindwa kutekeleza wajibu wake na kukufanya uandamane?
It is an outright illusion ...Haya ni Maandamano ya Amani yenye huzuni siyo Furaha moyoni.
TUKUTANE MBEZI. KATIBA MPYA
HUTUJAMALIZA.
Naam. Tutaanza utekelezaji wa Kusudio la Maandamano ya Amani yasiyo na Ukomo kwa kutoa Taarifa ya Kuandamana kwa Jeshi la Polisi Kama sheria inavyotaka hivi Karibuni. Moja ya Muongozo wa Maandamano ni Waraka wa Maaskofu wa Kanisa Katoliki.
Siku 19 zimebaki kureclaim haki ya kuiwajibisha Serikali.Tanganyika is coming back Tommorrow.
Kataa mkataba haramu wa TZ na DPW ,Ngorongoro Land is for the Maasai not Arabs,Katiba Mpya ni sasa siyo kesho kutwa.
Aluta continua
Hukumu ya Mahakama itasomwa tarehe 10 Mwezi 8 Mwaka 2023. Asanteni kwa kuja Asanteni kwa Maombi Yenu. Asanteni kwa kututia moyo. Hatuna hofu na tupo tayari kupambana kwa maslahi ya Tanganyika. Mungu yupo na amekisikia kilio chetu
BAK Mwabukusi
Shambani Busokelo.
Hivi JWTZ wanajukumu gani katika Uchaguzi? Au ndo Tume Huru ya Uchaguzi?JWTZ siyo kikundi cha kisiasa ni jeshi adilifu la wananchi wa TZ.Tumeharibu kwenye Dini? Tumeharibu kwenye Michezo? Tafadhali Jeshi liachwe lifanye majukumu ya Kikatiba.HILI NI JESHI LA WANANCHI SIYO WAGOMBEA
Bado siku 12 kuelekea Tamko la Maaandamano ya Amani, Kupinga Mkataba Haramu wa bandari na Kuitaka serikali Kuanzisha Mchakato wa Katiba Mpya Sasa.
#NoToDpWorld
#KatibaMpyaSasa
#StopMasaiEviction
Kusaidia harakati hii, please share. Tutatuma count down kila siku.
Tupo Singida Leo na Kamanda Ole Sosopi tunaendelea na uinjilishaji wa Madai ya Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi.IGA ni ujambazi wa Raslimali za Tanganyika na Ngorongoro is for Maasai . Dodoma stay tuned
Mutawajua kwa lugha na kauli zao...hawa ndo eti chama chao ni Cha demokrasia kinachopigiwa mfano...yani Hajui uhitaji wa Katiba mpya,haguswi na uhitaji wa Tume Huru..Haumizwi na madhila yanayowapata Wamaasai...hatikiswi na uuzwaji wa Raslimali za Tanganyika