Dazzy Elly Profile
Dazzy Elly

@AsajileDaniel

Followers
8K
Following
507K
Media
17
Statuses
238K

Hustling is my favorite game.

Mbeya, Tanzania
Joined December 2023
Don't wanna be here? Send us removal request.
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
12 hours
Kuwa mwanaume tajiri nayo ni tabu sana,ile kauli ya "je ukifa mapema itakuaje?" Inakua ni maombi ya wewe kufa mapema. Kuanzia ndugu zako,mkeo,watoto na vijakazi wako,wote wanakua wanawaza ukidondoka itakuaje? Ni ngumu sana kuwaziwa kwa upendo pesa ilipotawala. Good morning fam.
33
21
50
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
1 day
Hivi kazi ya wahariri kwenye vyombo vya habari ilibadilika?.Kiongozi anaweza kuongea uongo wa wazi kabisa na takwimu zipo wazi za kumkanusha lakini unakuta chombo cha habari kimetoa habari kama ilivyo - Uchawa ni mbaya sana. Imekua kero kuangalia na kusoma habari sasa. Good day.
16
22
39
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
1 day
Ukipata mtu anayeweza kushirikiana nawe kutatua tatizo ulilonalo basi jitahidi umshikilie kwa nguvu zote,huo ni upendo halisi,alikua na chaguo jepesi la kutafuta kilicho bora. Ubaya ni kuwa siku hizi msaada pekee unaothaminiwa ni pesa tu,tumesahau utu. Good morning fam.
51
39
87
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
2 days
Ndoa na mahusiano mengi vimekua ni killing agents. Watu wanapitia maumivu makali mno ambayo yanawaua taratibu kila siku zinapoenda. Kuishi na binadamu mwenye mapungufu kiasilia ni ngumu mno. Ukiuliza wengi walio kwenye ndoa wanaweza kukuambia bora wasingeingia. Good morning fam.
62
38
90
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
3 days
Ile kauli ya "Kua uyaone" ni kama huwa inabeba laana fulani maana ukishakua unaona kila rangi mpaka unaanza kujiuliza ndio haya niliyokua naambiwa niyaone,ukiwa mdogo unakua huwezi elewa maumivu wanayopitia watu wazima na unaona ni kawaida tu. Sio rahisi kuwa mkubwa. Gm fam.
45
38
87
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
4 days
Usiishi kwa kufuata mkumbo,macho na akili unavyo.Vitumie vyema. Angalia jamii uliyopo kisha tafakari,kati ya wewe na jamii yako je kipi kinahitaji mabadiliko? Jibu lako lifanyie kazi,kila kitu huanza ndani ya akili ya mtu mmoja tu.Jukumu letu kuleta maendeleo. Good morning fam.
39
46
91
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
5 days
Ni ngumu sana kupendwa kwa muonekano wa nje tu kama muonekano wako wa ndani ni mchafu,zaidi utaishia kutumika na kutupwa na kila akupatae. Ubora wa mtu haupimwi na muonekano wake wa nje bali wa ndani zaidi yani vile vitu visivyopoteza mvuto wala kuzeeka. Good morning fam.
47
42
88
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
6 days
Katika kuomba kwa Mungu, tunatakiwa kushukuru kwa tulivyo navyo kwanza na kuomba ulinzi juu yake na ndio inakuja kuomba vile tunavyo tamani kuwa navyo. Kumbuka pia kuwa Mungu anakupa vile unavyo stahili. May we have a blessed sunday and get what we deserve. Good morning fam.
55
32
83
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
7 days
Mpaka pale tutakapoacha uoga wa mabadiliko ndio tutakapopata viongozi sahihi ambao watakua ndio wanaogopa kutudanganya na kutuona hatuna akili. Sisi ndio waajiri wa viongozi na tunatakiwa tuwe na nguvu juu yao,uoga wetu unatutesa siku zote. We need to change. Blessed weekend.
18
17
54
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
7 days
Dada ukiamua kudate na mbaba na akawa anakuhudumia vizuri basi jifunze kuweka akiba na kujiongeza na biashara ndogo ndogo,haina maana kula bata kwenda mbele wakati mbele yako yenyewe huijui. Vijana wanalalama kuwa wababa wanaharibu mabinti,kumbe ni akili fupi za mabinti. Gm fam.
42
30
73
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
8 days
Pengine walipotushinda wazungu ni kwenye uaminifu, Africa ili ufanikiwe kitu chako inabidi usimamie mwenyewe,ukiweka mtu anawaza kuua kitu chako anufaike yeye.Wivu na chuki ni rafiki mkubwa wa umasikini. Wenzetu wanafuata mikataba iliyowekwa,sisi sasa dah. Good morning fam.
48
32
70
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
9 days
Kuzaliwa mzuri ni mipango ya Mungu na uwezo wa kuchaguana wa wazazi,kuutumia uzuri wako hilo unaachiwa wewe. Kuwa mzuri na kuwa wa thamani ni vitu viwili tofauti.Thamani inajengwa na mtu husika. Wengi wanakosea na kujikuta washakua malaya kudhani hawastahili kupata shida. Gm fam.
25
18
56
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
9 days
Nimejifunza kitu kutoka kwenye siasa. Mtu unaanza uongo,unauzoea na kuanza kuuishi,yanakua ndio maisha yako halisi.Mwisho wa siku unaanza kuuchukia ukweli na wasema ukweli.And that's madness.Huwa najiuliza wanaishi vipi na familia zao? Wanatengeneza vizazi gani?. Good morning fam.
39
19
61
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
10 days
Kuwa mke nalo sio jambo rahisi hata kidogo,unaweza salitiwa na ukateswa ndani ya ndoa ila ukisema utoke tu basi jamii nzima inakugeuka,mpaka wale ndugu zako wa damu.Thamani yako inapungua, wanaume nao watakua wanakupitia tu,hakuna wa malengo nawe. Ni mtihani. Good morning fam.
50
35
89
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
11 days
Mtu anayeweza kusikia/kuongea/kufuata ukweli bila kuangalia hisia zake kutokana na ushabiki/ufuasi basi huyo mtu amefaulu mtihani wa werevu na hekima. Shabiki wa timu,mfuasi wa chama na muumini wa dini.Hivi vitu vinaathiri mno uwezo wa kufikiri kwa watu wengi. Good morning fam.
51
40
97
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
12 days
Kila kitu unachokiona leo kilianza na wazo la mtu mmoja,kamwe usidharau uwezo wako na mawazo yako,walioweza walidhubutu kuchukua hatua ya kutoa kilicho kichwani na kukifanya uhalisia. Ukithubutu leo,kesho utakua unaongea kitu kingine.Iwe ufaulu au funzo. Do it. Good morning fam.
51
34
86
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
13 days
Mwisho wa siku wote tutaishi maisha chini ya utawaka utakaokuwepo wakati huo. Tusichukiane kisa mtazamo tofauti na wala tusiuane,maisha ni ya kila mtu. Kumbuka kuwa viongozi wa siku hizi wengi wachumia tu. Jamii yako ni muhim zaidi,tupendane. Good morning fam.
37
18
56
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
14 days
Hii kitu inaitwa depression ni ya kawaida tu ikiwa haijakukuta,kizazi hiki kina hili tatizo kwa kiasi kikubwa mno. Mambo ni mengi na hayaendi sawa. Mapenzi ya dhati nadra,kazi hazipo,biashara zinakufa,serikali mbovu,mitindo ya maisha hatarishi. Kuna usalama?. Good morning fam.
42
37
75
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
15 days
Ni ngumu sana kwa mtu anayejifanya anajua kila kitu kuendelea kushauriwa,hata wakiona unaelekea kupata hasara/madhara watakuacha ili uonje utamu wa ujuaji. Hakuna ajuaye kila kitu na kuna busara kubwa katika kusikiliza kuliko kuongea. Be open to new ideas. Good morning friends.
35
32
71
@AsajileDaniel
Dazzy Elly
16 days
Uwezo wa kufikiri + ubunifu ni janga kubwa lililojificha kwa nchi za kiafrika. Iwe maofisini,kwenye biashara mpaka shuleni na vyuoni,watu hawajihangaishi kutumia akili vizuri,ni copy and paste tu. Inahitaji mafikirio mapya katika zama mpya na mazingira mapya. Good morning fam.
40
24
67